Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MUSAADA KWA FAMILIA | KULEA WATOTO

Wakati Kijana Wako Anajiumiza Mwenyewe

Wakati Kijana Wako Anajiumiza Mwenyewe

TATIZO

Unatambua kwamba binti yako amekuwa akijiumiza mwenyewe kimakusudi. Unajiuliza, ‘Kufanya hivyo kunamaanisha nini?’ ‘Je, binti yangu anajaribu kujiua?’

Inaelekea kwamba jibu ni hapana. Hata hivyo, ikiwa binti yako anajiumiza mwenyewe, * ana lazima ya musaada. Unaweza kumusaidia namna gani? Kwanza, fikiria jambo ambalo labda linamuchochea kufanya hivyo. *

SABABU GANI JAMBO HILO LINATOKEA?

Je, kijana kujiumiza mwenyewe ni mutindo unaopendwa na vijana wengi? Bila shaka, vijana fulani wanaanza mutindo wa kujiumiza wenyewe kwa sababu wamesikia kwamba vijana wengine wanafanya hivyo. Hata ikiwa vijana wengine wanajiumiza kwa kuwa ni mutindo unaopendwa na wengi, wengi kati yao hawafanye hivyo kwa sababu hiyo. Kwa nini kuna tofauti kati ya sababu hizo mbili? Mara nyingi kijana anayejiumiza anafanya hivyo kwa siri na anasikia haya sana kwa sababu ya tabia hiyo ya kujiumiza mwenyewe. Celia  * aliye na miaka 20 anasema hivi: “Sikutaka mutu yeyote ajue jambo ambalo nilikuwa nikifanya. Nilificha vizuri vidonda vyangu ili watu wasivione.”

Je, kujiumiza ni njia tu ya kuvutia watu? Wengine wanaweza kujiumiza kwa sababu hiyo. Lakini vijana wanaojiumiza ambao tunazungumuzia katika habari hii wanajaribu kuficha tabia yao na hawajaribu kutumia vidonda ao michubuko yao ili kuvutia mutu yeyote. Hata hivyo, kijana mumoja aliyekuwa akijiumiza zamani anasema kwamba alitaka mutu fulani atambue jambo hilo ili aweze kumusaidia haraka zaidi.

Sababu gani basi watu wanajiumiza wenyewe? Sababu zinazowafanya vijana wajiumize ni nyingi, lakini sababu ya kweli ni kwamba kijana anasikia uchungu moyoni ambao ni vigumu kueleza kwa maneno. Katika kitabu chake kinachozungumuzia tabia ya kujikata (Cutting), muchunguzi wa afya ya akili Steven Levenkron anaeleza kuwa mutu anayejiumiza mwenyewe ni “mutu ambaye ameona kwamba maumivu ya mwili yanaweza kumusaidia kutunza maumivu ya moyoni.”

Mara nyingi kijana anayejiumiza anasikia uchungu moyoni ambao ni vigumu kueleza kwa maneno

Namna gani ikiwa unajilaumu mwenyewe? Kuliko kuendelea kuwazia kwamba kijana wako anajiumiza mwenyewe kwa sababu haukumulea vizuri, kazia akili daraka lako la kuwa muzazi muzuri kwa kumusaidia kijana wako aache tabia hiyo.

MAMBO AMBAYO UNAWEZA KUFANYA

Umutie moyo binti yako akuelezee mambo yanayomusumbua. Mashauri ambayo yanafuata yanaweza kusaidia.

Uwe mwenye kufariji. Ikiwa binti yako anakuelezea kwamba anajiumiza, ujikaze kuepuka kushituka ao kuogopa. Lakini, zungumuza kwa njia ya utulivu na yenye kufariji.​—Kanuni ya Biblia: 1 Wathesalonike 5:14.

Uliza maulizo ambayo hayaogopeshe. Kwa mufano, unaweza kusema hivi: “Ninajua kwamba mara nyingi haujisikie vizuri. Ni nini kinakusumbua zaidi?” ao “Ninaweza kufanya nini ili kukusaidia wakati unajisikia una wasiwasi ao unavunjika moyo?” ao “Unafikiri ninaweza kufanya jambo gani la maana sana ili kufanya uhusiano wetu uwe muzuri?” Sikiliza majibu yake bila kumukatiza.​—Kanuni ya Biblia: Yakobo 1:19.

Saidia binti yako atambue sifa zake nzuri. Kwa sababu wale wanaojiumiza wanakazia akili juu ya uzaifu wao, labda unaweza kumutia binti yako moyo atambue sifa zake nzuri. Unaweza hata kumuomba aandike mambo matatu hivi kuhusu sifa zake nzuri. Kijana mwanamuke anayeitwa Briana anasema hivi: “Kuandika mambo mazuri kujihusu kulinisaidia kutambua kwamba nina sifa nzuri.” *

Umutie binti yako moyo asali kwa Yehova Mungu. Biblia inasema hivi: ‘Mutupe mahangaiko yenu yote juu yake, kwa sababu yeye anawajali ninyi.’ (1 Petro 5:7) Lorena, aliye na miaka 17 anasema hivi: “Nilijikaza kumuambia Yehova Mungu mahangaiko yote yaliyokuwa katika moyo wangu, zaidi sana wakati nilishawishiwa kujiumiza mwenyewe. Jambo hilo lilinisaidia kujikaza sana kuacha tabia hiyo.”​—Kanuni ya Biblia: 1 Wathesalonike 5:17.

^ Kujiumiza mwenyewe ni tabia ambayo inamuchochea mutu kujitendea vibaya mwenyewe, iwe kwa kujikata, kujikwaruza, kujipiga, ao kwa kutumia njia nyingine yoyote ya kujiumiza.

^ Ijapokuwa katika habari hii tunazungumuza juu ya mutoto mwanamuke, kanuni zinazozungumuziwa zinahusu pia mutoto mwanaume.

^ Majina yamebadilishwa katika habari hii.

^ Mara nyingi, tabia ya kujiumiza inaonyesha kwamba mutu anashuka moyo ao ana tatizo lingine la akili ao la kimwili. Katika hali hizo, labda mutu huyo anaweza kuhitaji kusaidiwa na muganga. Gazeti Amuka! halipendekeze matunzo yoyote. Hata hivyo, Wakristo wanapaswa kuwa hakika kwamba matunzo yoyote wanayopata hayapingane na kanuni za Biblia.