Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mambo Yenye Biblia Inatuambia

Mambo Yenye Biblia Inatuambia

“Hii ndiyo historia ya mbingu na dunia wakati ziliumbwa.” (Mwanzo 2:4) Ile maneno inaonyesha kwa kifupi mambo yenye Biblia inasema juu ya namna ulimwengu na dunia vilianza. Mambo yenye Biblia inasema inapatana na mambo ya kweli ya sayansi? Fikiria mifano fulani.

Ku Mwanzo: Mbingu na dunia vinaumbwa

Ni kweli ulimwengu haukuwaka na mwanzo?

Mwanzo 1:1 inasema hivi: “Katika mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia.”

Kufikia katikati ya karne ya 20, wanasayansi wengi wenye kujulikana walikuwa wanaamini kama ulimwengu haukuwaka na mwanzo. Lakini mambo yenye wanasayansi wamevumbula hivi karibuni inaonyesha kama kwa kweli ulimwengu ulikuwaka na mwanzo.

Dunia ilikuwa namna gani ku mwanzo?

Mwanzo 1:2, 9 inaonyesha kama ku mwanzo dunia “haikukuwa na umbo na ilikuwa bila kitu.” Ilikuwa inafunikwa na maji.

Wanasayansi wa leo wanakubaliana na ile mawazo. Mwanabiolojia Patrick Shih anasema kama ku mwanzo dunia yetu ilikuwa na “angahewa yenye haina oksijeni, na namna ilikuwa ni tofauti na namna tunaionaka leo.” Gazeti Astronomy inasema hivi: “Uchunguzi wenye watu wamefanya leo unatusaidia tuelewe kama ku mwanzo Dunia ilikuwa inayala maji. Kulikuwa tu sehemu kidogo ya inchi kavu ao pengine haikukuwa.”

Namna angahewa yetu iko njo tu vile ilikuwaka tangu zamani?

Mwanzo 1:3-5 inaonyesha kama wakati mwangaza ulianza kuingia mu angahewa, vitu vyenye kutokeza ule mwangaza vilikuwa haviyaanza kuonekana ku dunia. Ni kisha njo jua na mwezi vilianza kuonekana muzuri ku dunia.​—Mwanzo 1:14-18.

Biblia haiseme kama vitu vyote vyenye uzima vyenye viko ku dunia viliumbwaka mu siku sita za saa 24

Kituo kimoja cha kutafuta habari (The Smithsonian Environmental Research Center) kinasema kama ku mwanzo angahewa yetu iliwezesha tu mwangaza wenye kupenya ufike ku dunia. Ile kituo inasema hivi: “Ku mwanzo, gaze yenye kuitwa metane ilikuwa inafunika dunia.” Kisha, “ile gaze ilipotea na anga ikakuwa bluu.”

Vitu vyenye uzima vilitokea katika mupangilio gani?

Mwanzo 1:20-27 inasema kama samaki, ndege, na wanyama wa inchi kavu waliumbwa kwanza na kisha wanadamu wakaumbwa. Wanasayansi wanaamini kama samaki wa kwanza walitokea miaka mingi mbele ya wanyama wa inchi kavu wa kwanza-kwanza, na kama wanadamu walitokea wakati murefu kisha.

Biblia haiseme kama vitu vyenye uzima haviwezi kubadilika kadiri wakati inapita

Biblia haiseme nini?

Watu fulani wanasema kama mawazo ya Biblia haipatane na mambo yenye wanasayansi wamevumbula mu siku zetu. Lakini mara mingi wanasemaka vile juu hawaelewe muzuri mambo yenye Biblia inasema.

Biblia haiseme kama ulimwengu ao dunia ilishakafanya tu miaka 6 000. Lakini, inasema tu kama dunia na ulimwengu viliumbwa “katika mwanzo.” (Mwanzo 1:1) Biblia haiseme kabisa kama kumepita miaka ngapi tangu wakati dunia na ulimwengu viliumbwa.

Biblia haiseme kama vitu vyote vyenye uzima vyenye viko ku dunia viliumbwaka mu siku sita za saa 24. Lakini, inatumia neno “siku” juu ya kuzungumuzia vipindi vya murefu vya wakati. Kwa mufano, inasema kama uumbaji wa ulimwengu wote muzima, kutia ndani “siku” sita za uumbaji zenye zinazungumuziwa mu Mwanzo sura ya 1 ulifanyika mu kipindi ya wakati yenye inaitwa “siku yenye Yehova * Mungu alifanya dunia na mbingu.” (Mwanzo 2:4) Njo maana kila siku mu zile “siku” sita za uumbaji zenye Mungu alitumia juu ya kuumba dunia inaweza kuwa ilikamata wakati murefu sana.

Biblia haiseme kama vitu vyenye uzima haviwezi kubadilika kadiri wakati inapita. Kitabu ya Mwanzo inasema kama wanyama waliumbwa “kulingana na aina yao.” (Mwanzo 1:24, 25) Mu Biblia neno “aina” iko na maana kubwa. Inatumiwa juu ya kuzungumuzia vikundi vikubwa-vikubwa vya vitu vyenye uzima vya namna mbalimbali. Ni kusema, mu “aina” moja munaweza kuwa namna mbalimbali ya viumbe vyenye uzima. Njo maana tunaweza kusema kama kadiri wakati inapita, mu “aina” moja kunaweza kuwa mabadiliko kati ya viumbe wa namna mbalimbali wenye kuishi pamoja.

Unawaza nini?

Vile tumetoka kuona, Biblia inaeleza mu njia ya mwepesi na bila kudanganyika namna ulimwengu ulianza, namna dunia ilikuwa ku mwanzo, na namna vitu vyenye uzima vilifikia kukuwa. Hauone kama Biblia inaweza pia kutusaidia kujua Ule mwenye aliumba vile vitu vyote? Encyclopædia Britannica inasema kama wazo ya kuwa kuko mutu fulani wa hali ya juu mwenye aliumba vitu vyenye uzima inapatana na mambo yenye wanasayansi wamevumbula. *

^ fu. 17 Yehova ni jina la Mungu kama vile inaonyeshwa mu Biblia.

^ fu. 20 Encyclopædia Britannica haiseme kama vitu vyenye uzima viliumbwaka.