Ona video zinazopatikana

Mungu Iko Fasi Yote?

Mungu Iko Fasi Yote?

Jibu ya Biblia

 Mungu anaweza kuona mambo yote na kutenda kila fasi kwenye anataka. (Mezali 15:3; Waebrania 4:13) Lakini, Biblia haiseme kama iko fasi yote, ao kama iko mu kila kitu. Inaonyesha kama Mungu ni mutu kabisa na iko na fasi kwenye anaishi.

  •   Mungu anakuwaka namna gani? Mungu ni roho. (Yohana 4:24) Hatuwezi kumuona. (Yohana 1:18) Mu Biblia muko maono mbalimbali kumuhusu Mungu. Mu ile maono yote, Mungu anaonyeshwaka na iko fasi moja, hapana fasi yote.​—Isaya 6:1, 2; Ufunuo 4:2, 3, 8.

  •   Mungu anaishi wapi? Biblia inasema kama Mungu iko na ‘makao yake mbinguni.’ (1 Wafalme 8:30) Ile inamaanisha kama Mungu haishi ku dunia ao fasi fulani mu ulimwengu, lakini anaishi mbinguni. Biblia inaonyesha kama wakati fulani malaika “waliingia ili kusimama mbele ya Yehova.” * Ile nayo inaonyesha kama Mungu iko na fasi kwenye anaishi.​—Yobu 1:6.

Vile Mungu haiko fasi yote, anaweza kunihangaikia kabisa?

 Ndiyo. Mungu anahangaikia sana kila mutu. Hata kama Mungu anaishi mbinguni, anaonaka watu, ku dunia, wenye wanapenda kabisa kumufurahisha na anawasaidiaka. (1 Wafalme 8:39; 2 Mambo ya Nyakati 16:9) Ona namna Yehova anaonyeshaka kama anahangaikia kabisa watumishi wake waaminifu:

  •   Wakati unasali: Wakati uko unasali, Yehova anakuwaka anakusikiliza.​—2 Mambo ya Nyakati 18:31.

  •   Wakati unavunjika moyo: “Yehova iko karibu na wale wenye kuvunjika moyo; anaokoa wale wenye kupondwa roho.”​—Zaburi 34:18.

  •   Wakati uko na lazima ya kuongozwa: Yehova atatumia Neno yake Biblia juu ya kukupatia “ufahamu na kukufundisha.”​—Zaburi 32:8.

Mawazo fulani yenye haiko ya kweli

 Watu fulani wanasemaka: Mungu iko mu vitu vyote vyenye aliumba.

 Kweli njo hii: Mungu haishi ku dunia wala fasi ingine mu ulimwengu. (1 Wafalme 8:27) Ni kweli kama nyota na vitu vingine vyenye Mungu aliumba “vinatangaza utukufu wa Mungu.” (Zaburi 19:1) Lakini, Mungu haishi mu vitu vyenye aliumbasawa vile tu muchoraji hakuwake anaishi mu picha yenye alichora. Ile picha inaweza kutusaidia kujua mambo fulani kuhusu mwenye aliichora. Vilevile, vitu vyenye kuwa mu ulimwengu vinatusaidia kujua “sifa [za Muumbaji] zenye hazionekane,” sawa vile nguvu, hekima, na upendo.​—Waroma 1:20.

 Watu fulani wanasemaka: Juu Mungu ajue mambo yote na juu akuwe Mweza-Yote, anapaswa kuwa fasi yote.

 Kweli njo hii: Roho takatifu ni nguvu yenye Mungu anatumiaka juu ya kutimiza mambo mbalimbali. Kupitia roho yake takatifu, Mungu anaweza kuona na kufanya jambo yoyote, fasi yoyote, na saa yoyote, bila yeye mwenyewe kuwa pale.​—Zaburi 139:7.

 Watu fulani wanasemaka: Zaburi 139:8 inafundisha kama Mungu iko fasi yote juu inasema hivi: “Kama ningepanda mbinguni, ungekuwa kule,Na kama ningetandika kitanda changu katika Kaburi, angalia! ungekuwa kule.”

 Kweli njo hii: Ile andiko haiko nazungumuzia fasi kwenye Mungu iko. Ni maneno ya mufano yenye inaonyesha tu kama hakuna fasi kwenye kuwa mbali sana kwenye kunaweza kuzuia Mungu atusaidie.

^ Biblia inaonyesha kama jina ya Mungu ni Yehova.