Ona video zinazopatikana

Makuta Njo Chanzo ya Mambo Yote ya Mubaya?

Makuta Njo Chanzo ya Mambo Yote ya Mubaya?

Jibu ya Biblia

 Hapana. Biblia haiseme kama makuta ni kitu ya mubaya, na kama njo chanzo ya mambo yote ya mubaya. Watu fulani wanasemaka kama Biblia inasema “feza [makuta] ni chanzo cha mambo ya mubaya.” Lakini Biblia haiseme vile. Inasema kama “kupenda feza ni chanzo cha mambo ya mubaya.”​—1 Timoteo 6:10.

 Biblia inasema nini juu ya makuta?

 Biblia inasema kama wakati makuta inatumiwa muzuri, inaweza kuletea mutu faida, na hata “ulinzi.” (Muhubiri 7:12) Zaidi ya ile, Biblia inapongeza wale wenye wanaonyesha wengine ukarimu kwa kuwapatia vitu mbalimbali na hata makuta.​—Mezali 11:25.

 Lakini inatushauria tusione makuta kuwa jambo ya maana zaidi mu maisha yetu. Inasema hivi: “Njia yenu ya maisha ikuwe bila upendo wa feza, wakati munatosheka na vitu vya sasa.” (Waebrania 13:5) Ile andiko inatufundisha kama tunapaswa kuwa na mawazo yenye usawaziko kuhusu makuta, na hatupaswe kufuatilia utajiri. Lakini tunapaswa kutosheka na mambo yenye tuko nayo lazima kabisa, ni kusema, chakula, manguo, na fasi ya kulala.​—1 Timoteo 6:8.

 Juu ya nini Biblia inatuambia tusipende makuta?

 Watu wenye pupa hawatapata uzima wa milele. (Waefeso 5:5) Juu ya nini? Juu pupa ni aina ya ibada ya sanamu ao ibada ya uongo. (Wakolosai 3:5) Zaidi ya ile, wakati watu wenye pupa wanajikaza sana kupata vitu vyenye wanatamani, mara mingi wanafanyaka mambo ya mubaya. Mezali 28:20 inasema hivi: “Mwenye anaharakisha kupata utajiri hatakosa kuwa na hatia.” Watu wenye pupa wanaweza hata kufanya mambo ya mubaya sana sawa vile kuogopesha watu, kunyanganya, kuiba, kubeba watu kinguvu, ao kuua.

 Hata kama kupenda makuta hakutufikishe ku ile mambo ya mubaya, kunaweza kuwa na matokeo ingine ya mubaya. Biblia inasema kama “wale wenye wameazimia kuwa matajiri wanaanguka katika jaribu na mutego na tamaa nyingi za upumbavu na zenye kuumiza.”​—1 Timoteo 6:9.

 Mashauri yenye Biblia inatoa kuhusu makuta inaweza kutuletea faida gani?

 Kama hatuvunje kanuni za Mungu ili kutafuta makuta, tutalinda heshima yetu na Mungu atatukubali na kutusaidia. Mungu anaahidi hivi wale wenye wanajikaza kumufurahisha: “Sitakuacha hata kidogo, na sitakutupa hata kidogo.” (Waebrania 13:5, 6) Tena, anatuhakikishia kama “mutu muaminifu atapata baraka nyingi.”​—Mezali 28:20.