Ona video zinazopatikana

Je, Shetani Iko Kabisa?

Je, Shetani Iko Kabisa?

Jibu la Biblia

 Ndiyo, Shetani iko kabisa. Biblia inasema kwamba yeye ni ‘mutawala wa ulimwengu huu,’ kiumbe cha kiroho aliyejifanya muovu na kumuasi Mungu. (Yohana 14:30; Waefeso 6:11, 12) Biblia inamufunua waziwazi kupitia majina fulani na maana ya majina hayo:

Shetani si kanuni fulani ao tabia fulani ya ubaya

 Watu fulani wanafikiri kwamba Shetani Ibilisi ni kanuni fulani tu ao tabia fulani mbaya inayopatikana ndani yetu. Lakini, Biblia inazungumuzia mazungumuzo kati ya Mungu na Shetani. Mungu ni mukamilifu, kwa hiyo haingewezekana azungumuze na sehemu moja ya ubaya iliyo ndani mwake. (Kumbukumbu 32:4; Ayubu 2:1-6) Pia, Shetani alimujaribu Yesu, ambaye hana zambi. (Mathayo 4:8-10; 1 Yohana 3:5) Kwa hiyo, Biblia inaonyesha kwamba Shetani iko kabisa wala si ubaya tu ulio katika wanadamu.

 Watu wengi hawaamini kwamba Shetani iko, je, hilo litushangaze? Hapana, kwa kuwa Biblia inasema kwamba Shetani anatumia ujanja ili kutimiza makusudi yake. (2 Wathesalonike 2:9, 10) Ujanja anaotumia sana ni ule wa kupofusha watu ili wasiamini kwamba yeye iko.—2 Wakorintho 4:4.

Mawazo ya uongo kuhusu Shetani

  Wazo la kutunga: Lusifero ni jina lingine la Shetani.

 Ukweli ni kwamba: Neno la Kiebrania ambalo Biblia fulani zinatafsiri kuwa “Lusifero” linamaanisha “mwenye kungaa.” (Isaya 14:12) Maandiko yanayozunguka andiko hilo yanazungumuzia wafalme wa Babiloni, ambao Mungu alinyenyekeza kwa sababu ya kiburi chao. (Isaya 14:4, 13-20) Maneno “mwenye kungaa” yalitumiwa ili kuchekelea mufalme wa Babiloni kisha kuanguka kwake.

 

 Ukweli ni kwamba: Shetani si mutumishi wa Mungu, lakini adui wake. Shetani Ibilisi anapinga watumishi wa Mungu na kuwasingizia.​—1 Petro 5:8; Ufunuo 12:10.