Ona video zinazopatikana

MUSAADA KWA AJILI YA FAMILIA | NDOA

Namna ya Kuacha Kazi “ku Kazi”

Namna ya Kuacha Kazi “ku Kazi”

 Juu ya teknolojia, watu wanaweza kukuita saa ni saa. Kwa hiyo, mukubwa wako wa kazi, wafanyakazi wenzako, ao watu wenye wanatafuta biashara yako wanaweza kutazamia kama utakuwa ku kazi kila wakati na kila siku. Lakini, ile inaweza kufanya ikuwe nguvu sana kwako kuwa na usawaziko kuhusu kazi, ni kusema kujua wakati ya kutumika, na wakati ya kuhangaikia mambo ingine mu maisha yako, kutia ndani ndoa yako.

 Mambo yenye unapaswa kujua

  •   Teknolojia inaweza kufanya utumie wakati mingi zaidi ku kazi kuliko kupitisha wakati pamoya na bibi ao bwana yako. Kila wakati wanaweza kukuita, ao kukutumia e-mail, ao ujumbe fulani wenye unahusu kazi wakati hauko ku kazi. Kwa hiyo, inaweza kuonekana kama unapaswa kuihangaikia palepale.

     “Kwa sasa inaonekana ni nguvu kupitisha wakati na familia kisha kurudia ku nyumba juu wakati unatoka ku kazi, njo wakati wanakutumiaka e-mails ao wanakuita kuhusu mambo ya kazi, kwa hiyo unahangaikia ile mambo kuliko kuhangaikia bibi ao bwana yako.”​—Jeanette.

  •   Juu ya kuwa na usawaziko kati ya kazi na maisha ya familia, inaomba kujikaza. Kama haufanye mipango fulani, utakuwa napitisha wakati mingi ku kazi kuliko kupitisha wakati pamoya na bibi ao bwana yako.

     “Kila mara bibi ao bwana yako njo anakuwaka wa kwanza kukosa kuhangaikiwa juu ya kuwaza hivi: ‘Oh, atanielewa. Atanisamehe. Nitapitisha wakati pamoya naye saa ingine.’”—Holly.

 Mashauri fulani ya kukusaidia ukuwe na usawaziko kuhusu kazi

  •   Uone ndoa yako kuwa ya maana sana. Biblia inasema hivi : “Aliowaunganisha Mungu, mutu asiwatenganishe.” (Matayo 19:6, La Sainte Bible en swahili de la R. D Congo) Kama hauwezi kuacha mutu fulani ‘akutenganishe’ na bibi ao na bwana yako, sasa juu ya nini uache kazi iwatenganishe?

     “Watu fulani wenye kutafuta biashara yako wanawazaka kama juu wao njo wanakuleteaka makuta, wanapaswa kukupata kila wakati yenye wako na weye lazima. Juu ninajua kama ndoa yangu ni ya maana sana, nawaambiaka kama sikuwake na wakati siku yenye situmike, lakini nitawaita kisha.”—Mark.

     Ujiulize hivi: ‘Matendo yangu inaonyesha kama naona ndoa yangu kuwa ya maana zaidi kuliko kazi yangu?’

  •   Kama inawezekana, ukatale kutumika zaidi. Biblia inasema: “Wenye kiasi wako na hekima.” (Mezali 11:2) Kama uko na usawaziko, ile itafanya ukatale kufanya kazi fulani, ao uambie mutu fulani aifanye ku fasi yako.

     “Niko plombier. Kama mutu fulani anapenda nimufanyie kazi fulani haraka, anahangaikaka sana. Kwa hiyo, kama siko tayari kufanya kazi yenye wananiomba niwafanyie, nawaambiaka kuhusu mwengine plombier mwenye anaweza kuwasaidia.”​—Christopher.

     Ujiulize hivi: ‘Nakuwaka tayari kukatala kufanya kazi ya zaidi kama bibi ao bwana yangu atajisikia sawa vile simuhangaikie? Bibi ao bwana yangu atakubaliana na miye?’

  •   Mupange wakati ya kupitisha pamoya. Biblia inasema hivi: “Kila kitu kiko na wakati wake wenye uliwekwa.” (Muhubiri 3:1) Wakati uko na mambo mingi ya kufanya ku kazi, ni jambo ya maana sana kupanga wakati ya kupitisha pamoya na bibi ao na bwana yako, na uhakikishe kama unafanya vile.

     “Mara mingi, wakati tuko na mambo mingi ya kufanya, tunapangaka wakati ili kukula pamoya mangaribi, ao kuenda tembea ku plage, na kule tunaweza kupitisha wakati pamoya bila kukengeushwa.”​—Deborah.

     Ujiulize hivi: ‘Napangaka wakati ili kumuhangaikia bibi ao bwana yangu? Bibi ao bwana yangu atawaza nini?’

  •   Ufunge vyombo vyako vya kielektroniki. Biblia inasema: “Muhakikishe mambo ya maana zaidi.” (Wafilipi 1:10) Wakati fulani unazimishaka vyombo vyako vya kielektroniki juu usikengeushwe wakati wanakutumia ujumbe fulani wa kazi ao wakati wanakuita juu ya mambo fulani ya kazi?

     “Niko najikaza sana nisiendelee kutumika kisha saa ya kazi. Ile wakati ikifika, nazimishaka telefone yangu.”​—Jeremy.

     Ujiulize hivi: ‘Nalazimikaka kuacha telefone yangu wazi juu tu mukubwa wangu wa kazi ao juu mutu fulani mwenye kunitafuta juu ya biashara yangu iko na lazima yangu? Bibi ao bwana yangu atakubaliana na miye?’’

  •   Ukuwe na usawaziko. Biblia inasema hivi: “Usawaziko wenu ujulikane kwa watu wote.” (Wafilipi 4:5) Kusema kweli, wakati fulani kazi inaweza kuvuruga ndoa yako. Kwa mufano, pengine kazi ya bibi ao ya bwana yako inamuomba atumike ao aongee ku telefone mambo yenye inahusu kazi kisha saa ya kazi. Ukuwe na usawaziko. Usimuombe bibi ao bwana yako mambo yenye inapita ile yenye anaweza kufanya.

     “Bwana yangu anafanyaka biashara fulani, na kila mara anakuwaka na mambo ingine ya kufanya kisha saa ya kazi. Wakati fulani, ile inanikasirishaka. Lakini juu tungali napitisha wakati pamoya, ile hainihangaishake kabisa.”—Beverly.

     Ujiulize hivi: ‘Juu najua kiasi ya kazi yenye bibi ao bwana yangu anafanyaka, najizuiaka nisimuombe wakati mingi ao anihangaikie sana kupita vile anaweza? Bibi ao bwana yangu atakubaliana na miye?’

 Maulizo ya kuzungumuzia

 Kwanza, munaweza kufikiria maulizo yenye kufuata kipekee. Kisha, muzungumuzie majibu.

  •   Bibi ao bwana yako alishakanungunika juu unaendelea kutumika ku nyumba? Kama ni vile, unakubaliana naye?

  •   Unawaza unaweza kufanya mabadiliko gani juu ukuwe na usawaziko kuhusu kazi?

  •   Ulishakajisikia sawa vile bibi ao bwana yako iko na magumu ya kuacha kazi “ku kazi”? Kama ni vile, unakumbuka wakati alikuwa mu ile hali?

  •   Ungependa bibi ao bwana yako afanye mabadiliko gani juu ya kuwa na usawaziko kuhusu kazi?