Ona video zinazopatikana

MUSAADA KWA AJILI YA FAMILIA

Mambo Yenye Wazazi Wanapaswa Kujua Kuhusu Kupeleka Mutoto Wao Fasi ya Kuchungia Watoto

Mambo Yenye Wazazi Wanapaswa Kujua Kuhusu Kupeleka Mutoto Wao Fasi ya Kuchungia Watoto

 Wazazi fulani wenye wanatumikaka wanatumaka watoto wao wenye hawayaanza masoma fasi ya kuchungia watoto. Ni fasi kwenye kunafanyikaka mambo ileile yenye inafanyikaka ku masomo. Ni muzuri kutuma mutoto wako kule?

 Maulizo yenye unapaswa kujiuliza

 Kama natuma mutoto wangu fasi ya kuchungia watoto, ile haitaharibisha uhusiano wenye kuwa kati yangu naye? Inaweza kuharibisha. Mu miaka ya kwanza-kwanza ya mutoto, ubongo wake unakomala haraka kadiri anapitisha wakati na wengine. Ujikaze kukuwa pamoya na mutoto yako mu hii kipindi ya maana sana yenye inaweza kuwa na matokeo fulani kwa mutoto wako mu maisha yake yote.​—Kumbukumbu la Torati 6:6, 7.

  •    Wazazi wenye wanafikiria kupeleka mutoto wao fasi ya kuchungia watoto wanapaswa kujiuliza watafanya nini juu waendelee kuwa na uhusiano wa karibu pamoya na mutoto wao.

 Kupeleka mutoto wako fasi ya kuchungia watoto kunaweza kumufanya asikusikilize tena? Inawezekana. Kitabu moya inasema hivi: “Kadiri watoto wenye hawayaanza masomo wanapitisha wakati pamoya, ni vile wanakuwaka na muelekeo wa kutenda sawa vile watoto wenzao.” (Hold On to Your Kids).

  •    Wazazi wenye wanafikiria kutuma mutoto wao fasi ya kuchungia watoto wanapaswa kujiuliza ikiwa wataendelea kuwa na mamlaka juu ya mutoto wao.

 Kupeleka mutoto wako fasi ya kuchungia watoto kutamusaidia wakati ataanza masomo? Watu fulani wanasema ndiyo. Na wengine wanasema kutamusaidia kidogo, ao hakutamusaidia. Penelope Leach, mutu mwenye elimu ya psikolojia anaandika hivi: “Musiwaze kama mambo yenye mutoto anajifunza ku masomo njo yenye itamusaidia kuwa na maisha ya muzuri, na musiwaze kama atakuwa tu na maisha ya muzuri juu alianza masomo na angali mudogo. Kama munawaza vile, mutazarau mambo yenye mulikuwa nafundisha mutoto wenu wakati angali mutoto.”

  •   Wazazi wenye wanafikiria kupeleka mutoto wao fasi ya kuchungia watoto wanapaswa kujiuliza kama iko na faida, ao kama ni lazima kufanya vile.

 Inawezekana bibi ao bwana akuwe nabakia na mutoto wenu ku nyumba kuliko kumupeleka fasi ya kuchungia watoto? Mu hali fulani, wazazi wote wawili wanatumikaka juu wakuwe na maisha ya muzuri. Ile iko na faida kabisa?

  •   Wazazi wenye wanafikiria kupeleka mutoto wao fasi ya kuchungia watoto wanaweza kuchunguza ikiwa inawezekana kupunguza garama fulani juu muzazi moya akuwe nabakia ku nyumba.

 Mbele ya kuamua kama utatuma mutoto wako fasi ya kuchungia watoto, unapaswa kufikiria kwa uzito faida na magumu ya kufanya vile. Kama kisha kufanya vile, unaona kama ni muzuri kutuma mutoto wako fasi ya kuchungia watoto, ni mambo gani ingine yenye unaweza kufikiria?

 Mambo yenye unaweza kufanya

 Biblia inasema hivi: “Mwerevu anafikiria sana kila hatua.” (Mezali 14:15) Kulingana na ile kanuni, tunapaswa kufikiri sana mbele ya kuamua kumupeleka mutoto yetu fasi ya kuchungia watoto.

 Fikiria njia mbalimbali za kuchunga watoto

  •   Wazazi fulani wanachaguaka kutuma mutoto wao fasi ya kuchungia watoto yenye kuwa mu nyumba ya mutu fulani. Mu ile nyumba, munaweza kuwa mutu moya ao watu fulani wa kuchunga watoto; na wanachungaka kikundi kidogo ya watoto.

  •   Wazazi wengine wanachaguaka mutu wa familia ao mutu fulani wa kuchunga watoto juu achunge mutoto wao.

 Kila njia iko na faida zake na magumu yake. Unaweza kuomba mashauri kwa wazazi wengine wenye walitumia njia fulani ya kuchunga watoto wao. Biblia inasema hivi: “Hekima ni ya wale wenye kutafuta shauri.”​—Mezali 13:10. . .

 Kama unaamua kutuma mutoto wako fasi ya kuchungia watoto, tafuta habari kuhusu ile fasi.

  •   Ile fasi inakubaliwa kisheria? Iko na sifa gani? Ao watu wanakuwaka na mawazo gani kuihusu?

  •   Iko safi na salama?

  •   Ni mambo gani watoto wanafanyaka kule? a

 Tafuta habari kuhusu wale wenye kuchunga watoto

  •   Ni masomo gani yenye walisoma? Uchunguze kama walisoma masomo ya kuchunga watoto, kama wanajua mambo ya kufanya ikiwa mutoto anaumia, na kama wako na uwezo wa kusaidia moyo wa mutoto uanze tena kupiga.

  •  Uchunguze pia kama wale wenye watachunga mutoto wako hawayatendeaka mubaya mutu fulani.

  •   Wanabadilishaka sana wafanyakazi? Kama wanafanyaka vile, itaomba kila mara mutoto wako akuwe najipatanisha na mufanyakazi wa mupya.

  •   Mufanyakazi moya anapaswa kuhangaikia watoto ngapi? Kama mufanyakazi moya anahangaikia watoto wengi, ni kusema mutoto wako hatahangaikiwa vile inaomba. Kusema kweli, namna mutoto wako anapaswa kuhangaikiwa inategemea miaka yake na uwezo wake.

  •   Wale wenye kuchunga mutoto wako wako tayari kuzungumuza na weye kuhusu mambo yenye inakuhangaisha ao mambo yenye inawahangaisha?

a Kwa mufano, kule mutoto wako atakuwa napitisha wakati mingi na iko naangalia televizyo ao watamusaidia ajifunze mambo fulani na kufanya mazoezi fulani ya mwili?