Ona video zinazopatikana

MUSAADA KWA AJILI YA FAMILIA | KUKOMALISHA WATOTO

Juu ya Nini Kusoma Ni Jambo ya Maana kwa Watoto​—Sehemu ya 2: Kusomea ku Karatasi ao ku Chombo ya Kielektroniki?

Juu ya Nini Kusoma Ni Jambo ya Maana kwa Watoto​—Sehemu ya 2: Kusomea ku Karatasi ao ku Chombo ya Kielektroniki?

 Mutoto wako anafurahiaka nini​—Kusoma mu kitabu yenye kuchapishwa ao mu chombo ya kielektroniki?

 Vijana wengi wanaweza kuchagua chombo ya kielektroniki. Dr. Jean M. Twenge anasema hivi: Kizazi yenye imezoea kuponda tu ku lien ao kupitisha ku ukurasa wa kufuata mu segonde kidogo tu, inaona kama kusoma vitabu ni jambo ya kuleta uvivu. a

 Kwa kweli, kusoma kwa kutumia chombo ya kielektroniki kuko na faida fulani. John mwenye kuwa na miaka 20 anasema hivi: “Kwenye nilisomea tulitumikisha vyombo vya kielekroniki. Sehemu ya kutafuta ilinisaidia nipate habari yenye nilikuwa nayo lazima.”

 Kuko faida zingine za mingi za kusomea mu vyombo vya kilektroniki. Kwa mufano, kama unaponda tu fasi fulani unaweza kupata maana ya neno, unaweza kusikiliza audio, unaweza kuangalia video yenye inapatana na ile habari, ao unaweza kusoma habari zaidi. Ni kusema hakuna faida ya kusoma vichapo vyenye kuchapishwa?

 Watu fulani wanapendelea kusomea ku karatasi wakati wanatafuta kujifunza kwa undani. Juu ya nini?

  •   Kukazia akili. Kijana mwenye kuitwa Nathan anasema hivi: “Wakati niko nasomea ku chombo ya kielektroniki, ujumbe unaweza kuingia, na mara mingi ile inanikengeusha na kufanya nisikazie akili mambo yenye niko nasoma.”

     Karen wa miaka 20, anapambana pia na ile tatizo. Anasema hivi: “Wakati niko nasomea ku telefone na ku tablette, ni mwepesi kwangu kukengeushwa na kuanza kutumia programu ingine, ao kuanza kucheza muchezo fulani.”

     Kanuni ya Biblia: “Mukitumia muzuri zaidi wakati wenu.”​—Kol. 4:5.

     Jambo ya kufikiria: Mutoto wako iko kabisa na uwezo wa kujizuia ili kuepuka vitu venye vinaweza kumukengeusha akili wakati iko nasoma ao kujifunza kwa kutumia chombo ya kielektroniki? Namna gani unaweza kumusaidia ili akazie akili mambo yenye iko najifunza?

     Pendekezo: Saidia mutoto wako aelewe kama vitu vya kukengeusha akili vyenye kuwa ku vyombo vya kielektroniki vitafanya asimalize mbio kazi za masomo, na kumukulia wakati wenye angefanya mambo ingine.

  •   Kuelewa. Kitabu moja inasema hivi: “Uchunguzi mbalimbali umeonyesha kama mwenye anasomea ku chombo ya kielektroniki na mwenye anasomea ku karatasi hawaelewake mambo mu njia ileille.”(Be the Parent, Please)

     Sababu moja ni kwamba mara mingi mutu mwenye anasomea ku chombo ya kielektroniki anasomaka mbio-mbio bila kufikiria mambo yenye iko nasoma. Muandikaji Nicholas Carr anasema hivi: “Wakati tuko nasoma habari ku Enternete, tunapendaka kusoma habari mingi mbio-mbio kadiri inawezekana.” b

     Wakati fulani kusoma mbio-mbio kunakuwaka na faida. Lakini Carr anasema kama shida ni kwamba “Ile njo inakuwa namna yetu ya kusoma.” Matokeo itakuwa nini? Mutoto wako atakuwa na tabia ya kusoma mambo mbio-mbio bila hata kuelewa mambo yenye iko nasoma.

     Kanuni ya Biblia: “Pamoja na vyote vyenye unapata, pata uelewaji.”​—Mez. 4:7.

     Jambo ya kufikiria: Nini njo inaweza kusaidia mutoto wako ajifunze zaidi habari ikuwe ku karatasi ao chombo ya kielektroniki?

     Pendekezo: Ukuwe na usawaziko. Haiko lazima utumie tu karatasi, ao utumie tu chombo ya kieletroniki. Zote ziko na faida. Na hata mambo fulani yenye kuwa mu vichapo vya kielektroniki inaweza kusaidia mutu aelewe habari muzuri zaidi. Kwa hiyo, ukuwe na usawaziko wakati uko nazungumuzia na watoto wako matokeo ya muzuri na matokeo ya mubaya ya kutumia aina yoyote ya kusoma. Ukumbuke pia kama kila mutoto iko tofauti.

  •   Kuweka mambo mu akili. Mu habari yenye ilitolewa mu Scientific American Ferris Jabr anasema kama, tofauti na vichapo vyenye kuchapishwa, vichapo vya kielektroniki “vinaweza kufanya ubongo wetu uchoke zaidi . . . na inaweza kuwa nguvu zaidi kwetu kukumbuka mambo yenye tulisoma.”

     Kwa mufano, kusomea mu kitabu kunaweza kukusaidia kukumbuka mambo, juu unajua ni ku ukurasa gani ulisoma jambo fulani. Ile inaweza kusaidia upate ile jambo wakati utakuwa tena nayo lazima.

     Zaidi ya ile, watu wenye kufanya uchunguzi wanaona kama wale wenye wanasomea ku vichapo vyenye kuchapishwa, wanakumbukaka muzuri zaidi mambo yenye walisoma. Wanaikumbukaka juu inaonekana walijifunza muzuri zaidi.

     Kanuni ya Biblia: “Linda hekima yenye kutenda na uwezo wa kufikiri.”​—Mez. 3:21.

     Jambo ya kufikiria: Inakuwaka nguvu kwa mutoto wako kuelewa ao kukumbuka mambo yenye alisoma ao kujifunza? Kama ni vile, unaweza kumusaidia akuwe najifunza muzuri zaidi? Kutumia vichapo vyenye kuchapishwa, kunaweza kusaidia?

     Pendekezo: Angalia jambo yenye inasiadia zaidi mutoto wako, hapana yenye anafurahia. Mara mingi inakuwaka mwepesi kwa watu kusema kama wanasomaka muzuri sana vya kielektroniki.

a Inatoka mu kitabu iGen.

b Inatoka mu kitabu The Shallows.