Hamia kwenye habari

Je, Mashahidi wa Yehova ni Wafuasi wa Dini ya Uyahudi?

Je, Mashahidi wa Yehova ni Wafuasi wa Dini ya Uyahudi?

 Hapana, si kweli. Mashahidi wa Yehova ni Wakristo ambao mafundisho yao yanategemea Maandiko. Ingawa dini fulani zinafundisha kwamba mikutano ya Wayahudi inayofanywa huko Palestina inahusiana na unabii wa Maandiko, Mashahidi wa Yehova hawaamini hivyo. Hawaamini kwamba mpango huo wa kisiasa ulitabiriwa kihususa na Maandiko. Kwa kweli, Maandiko hayaungi mkono serikali yoyote ya kibinadamu wala kutukuza jamii au kikundi fulani cha watu. Gazeti Mnara wa Mlinzi, ambalo ni gazeti rasmi la Mashahidi wa Yehova lilisema hivi waziwazi: “Hakuna msingi wowote wa Kimaandiko wa kuunga mkono siasa za Uyahudi.”

 Kitabu Encyclopædia Britannica kinafafanua Dini ya Uyahudi kuwa “Wanaharakati Wayahudi ambao lengo lao ni kuanzisha na kutegemeza taifa la Kiyahudi huko Palestina.” Msingi wao ni wa kidini na kisiasa. Mashahidi wa Yehova hawafundishi fundisho la Dini ya Uyahudi, na hawaungi mkono upande wowote inapohusu siasa za Dini ya Uyahudi.

 Shirika la Mashahidi wa Yehova ni la kidini kabisa na haliungi mkono mpango wowote wa kisiasa, kutia ndani Dini ya Uyahudi. Historia inaonyesha kwamba Mashahidi wa Yehova hawaungi mkono upande wowote wa kisiasa, na katika nchi fulani Mashahidi wamenyanyaswa vikali kwa kukataa kuunga mkono siasa. Tunasadiki kwamba Ufalme wa Mungu ulio mbinguni ndio utakaoleta amani ya kudumu duniani, hakuna serikali ya kibinadamu au wanaharakati wanaoweza kutimiza hilo.

 Mojawapo ya mafundisho ya msingi ya Mashahidi wa Yehova, popote wanapoishi, ni kutii sheria za serikali. Hawapingi mamlaka za kiserikali au kushiriki vita.