Kwa Waebrania 5:1-14

  • Yesu ni mkuu kuliko makuhani wakuu wanadamu (1-10)

    • Kwa mfano wa Melkizedeki (6, 10)

    • Alijifunza utii kutokana na mateso (8)

    • Ana daraka la kuleta wokovu wa milele (9)

  • Onyo dhidi ya kukosa ukomavu (11-14)

5  Kwa maana kila kuhani mkuu anayechaguliwa miongoni mwa wanadamu huwekwa rasmi kwa ajili yao juu ya mambo yanayohusiana na Mungu,+ ili atoe zawadi na dhabihu kwa ajili ya dhambi.+  Yeye anaweza kuwatendea kwa huruma* wale wasiojua na wanaokosea,* kwa sababu yeye pia anapambana* na udhaifu wake mwenyewe,  na hivyo ni lazima atoe dhabihu kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe kama vile anavyotoa kwa ajili ya dhambi za watu.+  Mtu hapati heshima hii kwa kupenda kwake mwenyewe, bali huipokea tu Mungu anapomwita, kama Haruni alivyoitwa.+  Vivyo hivyo, pia Kristo hakujitukuza mwenyewe+ kwa kuwa kuhani mkuu, bali alitukuzwa na Yule aliyemwambia hivi: “Wewe ni mwanangu; leo nimekuwa baba yako.”+  Kama vile pia anavyosema mahali pengine, “Wewe ni kuhani milele kwa mfano wa Melkizedeki.”+  Alipokuwa duniani,* Kristo alitoa dua na pia maombi, kwa vilio vyenye nguvu na machozi,+ kwa Yule aliyekuwa na uwezo wa kumwokoa kutoka katika kifo, naye akasikilizwa vizuri kwa sababu ya kumwogopa Mungu.  Ingawa alikuwa mwana, alijifunza kutii kutokana na mateso yaliyompata.+  Na baada ya kufanywa kuwa mkamilifu,+ akawa na daraka la wokovu wa milele kwa ajili ya wote wanaomtii,+ 10  kwa sababu Mungu amemteua kuwa kuhani mkuu kwa mfano wa Melkizedeki.+ 11  Tuna mengi ya kusema kumhusu na ni vigumu kuyafafanua, kwa sababu mmekuwa wazito wa kusikia. 12  Kwa maana, ingawa kufikia sasa* mnapaswa kuwa walimu, mnahitaji tena mtu awafundishe tangu mwanzo mambo ya msingi+ ya maneno matakatifu ya Mungu, nanyi mnahitaji maziwa tena, bali si chakula kigumu. 13  Kwa kuwa kila mtu anayeendelea kunywa maziwa hafahamu neno la uadilifu, kwa maana yeye ni mtoto mdogo.+ 14  Lakini chakula kigumu ni cha watu wakomavu, ambao wamezoeza nguvu zao za utambuzi* kwa kuzitumia ili kutofautisha mambo yaliyo sawa na mambo yasiyo sawa.

Maelezo ya Chini

Au “kwa wororo; kwa kiasi.”
Au “wasiotii.”
Au “anakabiliana.”
Tnn., “Katika siku za mwili wake.”
Tnn., “kulingana na wakati.”
Au “nguvu zao za ufahamu.”