Mambo ya Walawi 20:1-27

  • Ibada ya Moleki; kuwasiliana na roho waovu (1-6)

  • Iweni watakatifu na muwaheshimu wazazi (7-9)

  • Wanaofanya ngono haramu wanapaswa kuuawa (10-21)

  • Iweni watakatifu ili mwendelee kuishi nchini (22-26)

  • Wanaowasiliana na roho waovu wanapaswa kuuawa (27)

20  Yehova akaendelea kumwambia Musa:  “Waambie hivi Waisraeli: ‘Mwanamume yeyote Mwisraeli na mgeni yeyote anayeishi katika nchi ya Israeli atakayemtoa mtoto wake dhabihu kwa Moleki ni lazima auawe.+ Watu wote wanapaswa kumuua kwa kumpiga mawe.  Mimi mwenyewe nitamkataa* mtu huyo, nami nitamwangamiza, kwa sababu amemtoa mtoto wake dhabihu kwa Moleki, ametia unajisi mahali pangu patakatifu+ na kulichafua jina langu takatifu.  Watu wakimwona mtu huyo akimtoa mtoto wake dhabihu kwa Moleki na wakatae kimakusudi kumuua mtu huyo,+  basi mimi mwenyewe nitamkataa* mtu huyo pamoja na familia yake.+ Nitamwangamiza pamoja na wote waliojiunga naye kufanya ukahaba na Moleki.  “‘Kwa hakika nitamkataa na kumwangamiza mtu yeyote anayetafuta ushauri kutoka kwa watu wanaowasiliana na roho+ na pia wabashiri+ ili kufanya ukahaba wa kiroho pamoja nao.+  “‘Ni lazima mjitakase na kuwa watakatifu,+ kwa sababu mimi ni Yehova Mungu wenu.  Nanyi lazima mshike sheria zangu na kuzifuata.+ Mimi ni Yehova, ninayewatakasa.+  “‘Mtu yeyote anayemtukana* baba yake au mama yake lazima auawe.+ Kwa kuwa amemtukana baba yake au mama yake atakuwa na hatia kwa sababu ya kifo chake mwenyewe.* 10  “‘Ifuatayo ni sheria kuhusu mwanamume anayefanya uzinzi na mke wa mwanamume mwingine: Mwanamume anayefanya uzinzi na mke wa mwenzake lazima auawe; mwanamume huyo na mwanamke aliyefanya naye uzinzi lazima wauawe.+ 11  Mwanamume anayefanya ngono na mke wa baba yake amemwaibisha baba yake.*+ Ni lazima wote wawili wauawe. Watakuwa na hatia kwa sababu ya vifo vyao wenyewe.* 12  Mwanamume akifanya ngono na binti mkwe wake, wote wawili wanapaswa kuuawa. Wamekiuka sheria ya asili. Watakuwa na hatia kwa sababu ya vifo vyao wenyewe.*+ 13  “‘Mwanamume akilala na mwanamume mwenzake kama vile mwanamume anavyolala na mwanamke, wote wawili wamefanya jambo linalochukiza.+ Ni lazima wauawe. Watakuwa na hatia kwa sababu ya vifo vyao wenyewe.* 14  “‘Mwanamume akimwoa mwanamke na afanye ngono na mama ya mwanamke huyo, ni tendo chafu linalochukiza.*+ Anapaswa kuchomwa moto+ pamoja na wanawake hao, ili mwenendo huo mchafu unaochukiza usiendelee miongoni mwenu. 15  “‘Mwanamume akifanya ngono na mnyama lazima auawe, mnapaswa pia kumuua mnyama huyo.+ 16  Mwanamke akienda kufanya ngono na mnyama,+ ni lazima mumuue mwanamke huyo pamoja na mnyama huyo. Lazima wauawe. Watakuwa na hatia kwa sababu ya vifo vyao wenyewe.* 17  “‘Mwanamume akifanya ngono na dada yake, binti ya baba yake au binti ya mama yake na kuona uchi wake na binti huyo pia aone uchi wake, ni jambo la aibu.+ Ni lazima wauawe mbele ya watu wote. Amemwaibisha dada yake.* Anapaswa kuadhibiwa. 18  “‘Mwanamume akifanya ngono na mwanamke mwenye hedhi, mwanamume huyo na mwanamke huyo wamefunua mtiririko wa damu yake.+ Ni lazima wote wawili wauawe. 19  “‘Hupaswi kufanya ngono na dada ya mama yako au dada ya baba yako, kwa sababu kufanya hivyo ni kumwaibisha mtu wako wa ukoo uliye na uhusiano wa damu naye.+ Wanapaswa kuadhibiwa kwa sababu ya kosa lao. 20  Mwanamume anayefanya ngono na mke wa ndugu ya baba yake amemwaibisha* ndugu ya baba yake.+ Wanapaswa kuadhibiwa kwa sababu ya dhambi yao. Watakufa bila watoto. 21  Mwanamume akimchukua mke wa ndugu yake, ni jambo linalochukiza sana.+ Amemwaibisha ndugu yake.* Hawatazaa mtoto. 22  “‘Ni lazima mshike masharti yangu yote na sheria zangu zote+ na kuzifuata,+ ili nchi ninayowapa mwishi ndani yake isiwatapike.+ 23  Hampaswi kufuata sheria za mataifa ninayoyafukuza kutoka mbele yenu;+ kwa sababu yamefanya mambo hayo yote, nami ninayachukia kabisa mataifa hayo.+ 24  Ndiyo sababu niliwaambia: “Mtaimiliki nchi yao, nami nitawapa iwe miliki yenu, nchi inayotiririka maziwa na asali.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu, nami nimewatenga na mataifa mengine.”+ 25  Ni lazima mtofautishe mnyama aliye safi na asiye safi na ndege aliye safi na asiye safi;+ msinifanye niwachukie kwa kula mnyama au ndege au kiumbe yeyote anayetambaa niliyewaambia kwamba si safi.+ 26  Ni lazima muwe watakatifu mbele zangu, kwa sababu mimi, Yehova, ni mtakatifu,+ nami ninawatenga na mataifa mengine ili muwe watu wangu.+ 27  “‘Mwanamume au mwanamke yeyote ambaye anawasiliana na roho au ni mbashiri* lazima auawe.+ Watu wanapaswa kuwaua kwa kuwapiga mawe. Watakuwa na hatia kwa sababu ya vifo vyao wenyewe.’”*

Maelezo ya Chini

Tnn., “nitaukaza uso wangu dhidi ya.”
Tnn., “nitaukaza uso wangu dhidi ya.”
Tnn., “damu yake itakuwa juu ya kichwa chake.”
Au “anayemlaani.”
Tnn., “amefunua uchi wa baba yake.”
Tnn., “Damu yao itakuwa juu ya vichwa vyao.”
Tnn., “Damu yao itakuwa juu ya vichwa vyao.”
Tnn., “Damu yao itakuwa juu ya vichwa vyao.”
Au “ni mwenendo wa aibu; mwenendo mchafu uliopotoka.”
Tnn., “Damu yao itakuwa juu ya vichwa vyao.”
Tnn., “Amefunua uchi wa dada yake.
Tnn., “amefunua uchi wa.”
Tnn., “Amefunua uchi wa ndugu yake.”
Au “ana roho ya ubashiri.”
Tnn., “Damu yao itakuwa juu ya vichwa vyao.”