Kumbukumbu la Torati 4:1-49

  • Waagizwa watii (1-14)

    • Msisahau matendo ya Mungu (9)

  • Yehova anataka aabudiwe yeye peke yake (15-31)

  • Hakuna Mungu mwingine ila Yehova (32-40)

  • Majiji ya makimbilio upande wa mashariki wa Yordani (41-43)

  • Wapewa Sheria (44-49)

4  “Sasa, enyi Waisraeli, sikilizeni masharti na sheria ambazo* ninawafundisha kushika, ili mwishi+ na kuingia kuimiliki nchi ambayo Yehova, Mungu wa mababu zenu, anawapa ninyi.  Hampaswi kuongeza jambo lolote kwenye neno ninalowaamuru, wala kuondoa jambo lolote kutoka katika neno hilo,+ ili mzishike amri za Yehova Mungu wenu ninazowaamuru ninyi.  “Macho yenu wenyewe yameona mambo ambayo Yehova alitenda kuhusiana na kisa cha Baali wa Peori; Yehova Mungu wenu alimwangamiza kila mtu miongoni mwenu aliyemfuata Baali wa Peori.+  Lakini ninyi mnaoshikamana kabisa na Yehova Mungu wenu, nyote mko hai leo.  Tazameni, nimewafundisha masharti na sheria,*+ kama nilivyoamriwa na Yehova Mungu wangu, ili mzishike katika nchi mtakayomiliki.  Ni lazima mzifuate kwa uangalifu,+ kwa sababu watu watakaosikia kuhusu masharti haya yote wataona kwamba mna hekima+ na uelewaji,+ nao watasema, ‘Kwa hakika watu wa taifa hili kubwa wana hekima na uelewaji.’+  Kwa maana ni taifa gani kubwa ambalo miungu yake iko karibu nalo kama Yehova Mungu wetu alivyo karibu nasi wakati wowote tunapomlilia?+  Na ni taifa gani kubwa ambalo lina masharti ya uadilifu na sheria* kama Sheria hii yote ninayoweka mbele yenu leo?+  “Ila tu muwe waangalifu na kujihadhari sana, ili msisahau mambo ambayo macho yenu yameona na ili yasiondoke moyoni mwenu siku zote za maisha yenu. Ni lazima pia muwaambie wana wenu na wajukuu wenu.+ 10  Siku ambayo mlisimama mbele za Yehova Mungu wenu kule Horebu, Yehova aliniambia, ‘Wakusanye watu mbele zangu ili niwafanye wasikie maneno yangu,+ ili wajifunze kuniogopa+ siku zote ambazo watakuwa hai juu ya ardhi na ili wawafundishe wana wao.’+ 11  “Basi mlikaribia na kusimama chini ya mlima, na mlima huo ulikuwa ukiwaka moto uliofika mpaka mbinguni; kulikuwa na giza, wingu, na utusitusi mzito.+ 12  Yehova akaanza kuzungumza nanyi kutoka katika moto.+ Mlisikia maneno, lakini hamkuona umbo lolote+—kulikuwa na sauti tu.+ 13  Naye akawatangazia agano lake,+ alilowaamuru mshike—zile Amri Kumi.*+ Kisha akaziandika kwenye mabamba mawili ya mawe.+ 14  Wakati huo, Yehova aliniamuru niwafundishe masharti na sheria ambazo * mnapaswa kushika katika nchi mtakayoingia kuimiliki. 15  “Kwa hiyo, jihadharini sana—kwa sababu hamkuona umbo lolote siku ambayo Yehova alizungumza nanyi kule Horebu kutoka katikati ya moto— 16  ili msitende upotovu kwa kujitengenezea sanamu ya kuchongwa yenye umbo la mfano wowote, mfano wa mwanamume au mwanamke,+ 17  mfano wa mnyama yeyote duniani au mfano wa ndege yeyote anayeruka angani,+ 18  mfano wa kitu chochote kinachotambaa ardhini au mfano wa samaki yeyote aliye ndani ya maji chini ya dunia.+ 19  Nanyi mnapoinua macho yenu kutazama mbinguni na kuona jua na mwezi na nyota—jeshi lote la mbinguni—msishawishiwe kuviinamia na kuviabudu.+ Yehova Mungu wenu amewapa watu wote duniani* vitu hivyo. 20  Lakini ninyi ndio watu ambao Yehova aliwatoa katika tanuru la kuyeyushia chuma, kutoka Misri, ili muwe watu ambao ni mali yake*+ mwenyewe, kama mlivyo leo. 21  “Yehova alinikasirikia kwa sababu yenu,+ akaapa kwamba sipaswi kuvuka Yordani au kuingia katika nchi nzuri ambayo Yehova Mungu wenu anawapa iwe urithi wenu.+ 22  Kwa maana nitakufa katika nchi hii; sitavuka Yordani,+ lakini ninyi mtavuka na kuimiliki nchi hiyo nzuri. 23  Iweni waangalifu msisahau agano la Yehova Mungu wenu ambalo alifanya pamoja nanyi,+ na msijitengenezee sanamu ya kuchongwa, umbo la kitu chochote mlichokatazwa na Yehova Mungu wenu.+ 24  Kwa maana Yehova Mungu wenu ni moto unaoteketeza,+ Mungu anayetaka watu wamwabudu yeye peke yake.+ 25  “Ikiwa mtazaa wana na wajukuu na kuishi kwa muda mrefu nchini nanyi mtende upotovu na kutengeneza sanamu ya kuchongwa+ ya aina yoyote na kutenda uovu machoni pa Yehova Mungu wenu na hivyo kumkasirisha,+ 26  nachukua mbingu na dunia ili ziwe mashahidi dhidi yenu leo ya kwamba kwa hakika mtaangamia haraka kutoka katika nchi mnayovuka Yordani kwenda kuimiliki. Hamtaishi kwa muda mrefu katika nchi hiyo, badala yake mtaangamizwa kabisa.+ 27  Yehova atawatawanya miongoni mwa mataifa,+ na ni watu wachache tu kati yenu watakaookoka+ miongoni mwa mataifa ambayo Yehova atawafukuza ninyi mwende miongoni mwao. 28  Huko mtalazimika kuiabudu miungu ya miti na mawe iliyotengenezwa kwa mikono ya wanadamu,+ miungu ambayo haiwezi kuona wala kusikia wala kula wala kunusa. 29  “Mkimtafuta Yehova Mungu wenu mkiwa huko, hakika mtampata,+ naam, mkiutafuta ushauri wake kwa moyo wenu wote na kwa nafsi* yenu yote.+ 30  Baadaye mtakapokuwa mkiteseka sana na mambo hayo yote yatakapokuwa yamewapata, ndipo mtakapomrudia Yehova Mungu wenu na kuisikiliza sauti yake.+ 31  Kwa maana Yehova Mungu wenu ni Mungu mwenye rehema.+ Hatawaacha wala kuwaangamiza wala kusahau agano alilowaapia mababu zenu.+ 32  “Sasa, ulizeni kuhusu siku za zamani kabla ya ninyi kuwepo, tangu siku ambayo Mungu alimuumba mwanadamu duniani; tafuteni kuanzia mwisho mmoja wa mbingu mpaka mwisho mwingine wa mbingu. Je, kuna jambo lolote kubwa kama hili ambalo limewahi kutokea au kuna jambo lolote kama hili ambalo limewahi kusikiwa?+ 33  Je, kuna taifa lingine lolote ambalo limewahi kusikia sauti ya Mungu ikisema kutoka katika moto kama ninyi mlivyosikia na kuendelea kuishi?+ 34  Au je, Mungu amewahi kujaribu kujichukulia taifa kutoka kati ya taifa lingine kwa hukumu,* kwa ishara, kwa miujiza,+ kwa vita,+ kwa mkono wenye nguvu,+ kwa mkono ulionyooshwa, na kwa matendo ya kutisha,+ kama Yehova Mungu wenu alivyowafanyia kule Misri mbele ya macho yenu wenyewe? 35  Ninyi wenyewe mmeonyeshwa mambo hayo ili mjue kwamba Yehova ndiye Mungu wa kweli;+ hakuna mwingine isipokuwa yeye.+ 36  Aliwawezesha kusikia sauti yake kutoka mbinguni ili awarekebishe, na duniani aliwawezesha kuona moto wake mkubwa, na maneno yake mliyasikia kutoka katika moto.+ 37  “Kwa sababu aliwapenda mababu zenu na amechagua uzao wao* baada yao,+ naye aliwatoa Misri kwa nguvu zake kuu mbele ya macho yake. 38  Naye aliyafukuza kutoka mbele yenu mataifa makubwa zaidi na yenye nguvu zaidi kuliko ninyi, ili awalete ninyi katika nchi yao na kuwapa iwe urithi wenu, kama ilivyo leo.+ 39  Kwa hiyo, siku ya leo, mjue na kutia moyoni kwamba Yehova ndiye Mungu wa kweli juu mbinguni na chini duniani.+ Hakuna mwingine.+ 40  Ni lazima mshike masharti yake na amri zake ninazowapa ninyi leo, ili mambo yawaendee vyema ninyi na wana wenu baada yenu, ili mwendelee kuishi kwa muda mrefu katika nchi ambayo Yehova Mungu wenu anawapa.”+ 41  Wakati huo Musa alitenga majiji matatu upande wa mashariki wa Yordani.+ 42  Mtu yeyote anayemuua mwenzake bila kukusudia na hakuwa akimchukia,+ ni lazima akimbilie katika mojawapo ya majiji hayo ili aishi.+ 43  Majiji hayo ni Beseri+ kule nyikani katika uwanda wa juu kwa ajili ya watu wa kabila la Rubeni, Ramothi+ kule Gileadi kwa ajili ya watu wa kabila la Gadi, na Golani+ kule Bashani kwa ajili ya watu wa kabila la Manase.+ 44  Basi hiyo ndiyo Sheria+ ambayo Musa aliwapa Waisraeli. 45  Hivyo ndivyo vikumbusho, masharti, na sheria ambazo* Musa aliwapa Waisraeli baada ya kutoka Misri,+ 46  katika eneo la Yordani, kwenye bonde lililo ng’ambo ya Beth-peori,+ katika nchi ya Mfalme Sihoni wa Waamori, aliyekuwa akikaa Heshboni,+ ambaye Musa na Waisraeli walimshinda walipotoka Misri.+ 47  Nao wakaimiliki nchi yake na nchi ya Mfalme Ogu+ wa Bashani, wafalme wawili wa Waamori waliokuwa katika eneo lililokuwa upande wa mashariki wa Yordani, 48  kuanzia Aroeri,+ kwenye ukingo wa Bonde la Arnoni, mpaka Mlima Sioni, yaani, Hermoni,+ 49  na eneo lote la Araba upande wa mashariki wa Yordani, mpaka Bahari ya Araba,* chini ya miteremko ya Pisga.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “maamuzi ya hukumu ambayo.”
Tnn., “maamuzi ya hukumu.”
Tnn., “maamuzi ya hukumu.”
Tnn., “yale Maneno Kumi.”
Tnn., “maamuzi ya hukumu ambayo.”
Tnn., “walio chini ya mbingu.”
Au “urithi wake.”
Angalia Kamusi.
Au “majaribu.”
Tnn., “mbegu yao.”
Tnn., “maamuzi ya hukumu ambayo.”
Yaani, Bahari ya Chumvi.