Hamia kwenye habari

Je, Biblia Ni Kitabu Chenye Hekima ya Wanadamu?

Je, Biblia Ni Kitabu Chenye Hekima ya Wanadamu?

Jibu la Biblia

 Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ina maneno mengi ya hekima. Hata hivyo, ona jinsi inavyosema: “Andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu.” Kuna uthibitisho mwingi unaounga mkono jambo hilo. Fikiria mambo yafuatayo:

  •   Hakuna mtu ambaye amefaulu kupinga usahihi wa historia ya Biblia.

  •   Waandishi wa Biblia walikuwa wanaume wanyoofu ambao waliandika bila kupendelea. Unyoofu wao unathibitisha kwamba maandishi yao ni ya kweli.

  •   Biblia ina kichwa kimoja kikuu: kutetewa kwa haki ya Mungu ya kutawala wanadamu na utimizo wa kusudi lake kupitia Ufalme wake wa Mbinguni.

  •   Ingawa iliandikwa maelfu ya miaka iliyopita, Biblia haina mawazo ya uwongo ya kisayansi ambayo yalikubaliwa na watu wengi nyakati za kale.

  •   Hati za kihistoria zilizoandikwa zinathibitisha kwamba unabii wa Biblia, au utabiri wake, ulitimizwa.