Hamia kwenye habari

Broshua Kuhusu Habari za Ulimwenguni Pote

 

Mashahidi wa Yehova-Ni Nani?

Maelezo mafupi kuhusu Mashahidi wa Yehova—utendaji wao na utaratibu wanaofuata.

Mashahidi wa Yehova na Machapisho Yao

Machapisho ya Mashahidi wa Yehova yanapatikana kwenye mtandao na nakala zilizochapishwa zinapatikana pia. Machapisho hayo yanawasaidia watu kumkaribia Mungu na kuelewa vizuri zaidi mafundisho ya Biblia. Isitoshe, yanawasaidia wasomaji kuwa na mtazamo mzuri na yanaweza kuboresha maisha yao.

Mashahidi wa Yehova na Sehemu yao Katika Jamii

Mashahidi wa Yehova hujitahidi kutoa mchango wao katika jamii kwenye maeneo wanamoishi kwa kuendeleza elimu ya Biblia na pia kutoa misaada ya kibinadamu.

Mashahidi wa Yehova na Huduma yao ya Hadharani

Sehemu muhimu ya ibada ya Mashahidi wa Yehova ni kuwaeleza wengine ujumbe wa habari njema kutoka kwenye Biblia. Wanatumia njia zipi kufanya hivyo na jamii inanufaikaje kutokana na huduma hiyo?

Mashahidi wa Yehova na Maisha ya Familia

Mashahidi wa Yehova hujitahidi kutumia kanuni za Biblia katika familia zao na kufanya hivyo kunaleta manufaa kwa mume, mke, na watoto. Matokeo ni kwamba kunakuwa na usalama na upendo katika familia. Wazazi wanachukua kwa uzito wajibu wa kuwafundisha watoto wao viwango vya Biblia.

Mashahidi wa Yehova-Maswali Yanayoulizwa Mara Nyingi

Pata majibu kwa maswali kumi yanayoulizwa mara nyingi kuhusu Mashahidi wa Yehova.

Mashahidi wa Yehova na Afya

Mashahidi wa Yehova wanauona uhai kuwa zawadi yenye thamani kutoka kwa Mungu. Wanauona uhai na pia damu kuwa takatifu. Wanatafuta matibabu bora kabisa kwa ajili ya familia zao na wako tayari kushirikiana na wataalamu wa kitiba ili kupata matibabu mazuri na yaliyo salama ambayo yanaweza kutumiwa badala ya damu.

Mashahidi wa Yehova na Utumishi wa Badala wa Kiraia

Kwa muda mrefu, sheria za kimataifa zimekubali haki ya msingi ya kukataa utumishi wa kijeshi kwa sababu ya dhamiri. Mashahidi wa Yehova wanathamini sana serikali zinapofuata viwango vya kimataifa na kuandaa utumishi wa badala wa kiraia ambao si adhabu na ambao unanufaisha jamii.

Mashahidi wa Yehova na Kutojihusisha Katika Siasa

Mashahidi wa Yehova wanatenda kulingana na mafundisho ya Biblia wanapokataa kuunga mkono upande wowote wa kisiasa. Serikali nyingi zinatambua kwamba msimamo huo wa Mashahidi huchangia amani. Serikali hizo pia zinakubali kwamba Mashahidi wa Yehova ni raia wanaotii sheria na wanaowaheshimu wenye mamlaka na kushirikiana nao.

Mashahidi wa Yehova na Kukusanyika ka Ajili ya Ibada

Mashahidi wa Yehova wanaona kukutana na waabudu wenzao kuwa sehemu muhimu sana ya ibada yao. Kwa kawaida, mikutano yao inafanywa kwenye majengo yanayoitwa Majumba ya Ufalme. Mikutano hiyo inakazia hasa elimu ya Biblia na watu wote wanaweza kuhudhuria.

Mashahidi wa Yehova na Kutoa Msaada Wakati wa Majanga

Majanga yanapotokea, Mashahidi wa Yehova wanatenda kwa uharaka ili kuandaa msaada wa kimwili, kihisia, na kiroho. Jitihada zao zilizopangwa kwa utaratibu mzuri zinatambuliwa na idara mbalimbali serikalini pamoja na mashirika ya kutoa msaada.

Mashahidi wa Yehova wa Moscow na Wengine Dhidi ya Urusi

Muhtasari wa uamuzi wa Mahakama ya Ulaya ya Haki za Kibinadamu uliounga mkono Jamii ya Mashahidi wa Yehova wa Moscow.

Shirika la Kidini la Mashahidi wa Yehova la Taganrog na Wengine Dhidi ya Urusi

Muhtasari wa hukumu ya Mahakama ya Ulaya ya Haki za Kibinadamu katika kesi ya Shirika la Kidini la Mashahidi wa Yehova la Taganrog na Wengine Dhidi ya Urusi iliyotangaza kwamba ni kinyume cha sheria kwa Urusi kuwapiga marufuku Mashahidi wa Yehova.

Msimamo wa Kimaandiko wa Mashahidi wa Yehova Kuhusu Kuwalinda Watoto

Mashahidi wa Yehova wanazingatia sana haki za watoto. Sehemu hii inaeleza hatua zinazochukuliwa na Mashahidi wa Yehova dhidi ya madai ya kumtendea vibaya mtoto.