Hamia kwenye habari

Kushoto: Ndugu Yevgeniy Stefanidin. Kulia: Ndugu Aleksandr Votyakov

APRILI 23, 2024
URUSI

Tunathamini Sana Pendeleo la Kumtumikia Yehova

Tunathamini Sana Pendeleo la Kumtumikia Yehova

Mahakama ya Pervomayskiy iliyo katika Wilaya ya Izhevsk katika Jamhuri ya Udmurtian, itatangaza uamuzi wake katika kesi inayowahusu Ndugu Yevgeniy Stefanidin na Ndugu Aleksandr Votyakov. Mwendesha mashtaka bado hajatoa ombi la hukumu anayopendekeza.

Maelezo Mafupi Kuwahusu

Kama Aleksandr na Yevgeniy, tunaliona kuwa pendeleo kubwa “Kumtolea [Yehova] utumishi mtakatifu bila woga” siku zetu zote.​—Luka 1:74, 75.

Mfuatano wa Matukio

  1. Aprili 14, 2021

    Maofisa wa usalama walifanya msako kwenye nyumba ya Yevgeniy

  2. Desemba 13, 2022

    Kesi ya uhalifu ilifunguliwa dhidi ya Aleksandr na Yevgeniy

  3. Desemba 14, 2022

    Maofisa walifanya msako kwenye nyumba ya Aleksandr na ya Yevgeniy. Aleksandr alipelekwa mahabusu. Yevgeniy aliwekewa vizuizi vya kusafiri

  4. Desemba 15, 2022

    Aleksandr aliachiliwa kutoka mahabusu na akawekwa katika kifungo cha nyumbani

  5. Juni 9, 2023

    Aleksandr aliachiliwa kutoka katika kifungo cha nyumbani na akawekewa vizuizi vya kusafiri

  6. Agosti 17, 2023

    Kesi ya uhalifu ilianza