Ona video zinazopatikana

Walivala Triangle ya Rangi ya Zambarau

Walivala Triangle ya Rangi ya Zambarau

 Maud anaishi Ufaransa na anatumikaka ku masomo. Kazi yake ni kusaidia watoto walemavu wakati ya masomo. Kumepita siku kidogo wanafunzi wa somo fulani walikuwa najifunza kuhusu mauaji makubwa ya Wayahudi na kuhusu kambi za mateso za Wanazi. Ku nguo ya wafungwa wa mu zile kambi kulishonewa kipande ya nguo ya rangi ya zambarau. Rangi na umbo ya ile kipande ya nguo ilionyesha kama ule mutu alikuwa mufungwa.

 Wakati alizungumuzia kipande ya nguo ya umbo ya triangle ya rangi ya zambarau yenye wafungwa fulani walivala, ule mwalimu alisema hivi: “Niliwaza walivala vile juu walikuwa wanaume wenye wanalalaka na wanaume wenzao ao wanamuke wenye wanalalaka na wanamuke wenzao.” Kisha masomo, Maud alizungumuza na ule mwalimu na alimufasiria kama Wanazi walitumia triangle ya rangi ya zambarau ili kuonyesha kama wale ni Mashahidi wa Yehova. * Alimuuliza pia kama anaweza kumuletea habari fulani yenye kuzungumuzia ile jambo. Ule mwalimu alikubali, na alimuambia Maud aambie wanafunzi juu ya ile habari.

 Wakati ya ile habari ilizungumuziwa tena, mwalimu mwingine alitumia karte fulani ili kuonyesha alama mbalimbali zenye wafungwa walikuwa wanavala. Ile karte ilionyesha kabisa kama wale wenye walivala triangle ya rangi ya zambarau ni Mashahidi wa Yehova. Kisha masomo, Maud alipatia ule mwalimu habari fulani yenye kuzungumuzia ile jambo. Ule mwalimu alikubali na alifanya mipango juu Maud aambie wanafunzi juu ya ile habari.

Maud iko na vichapo vyenye alitumia

 Maud alitayarisha kipindi ya kufundisha wanafunzi wa somo ya kwanza mu dakika 15. Ule mwalimu alimuambia hivi: “Unaweza kutumia saa yote yenye ningetumia juu ya kufundisha.” Maud alianza kuonyesha video yenye kuonyesha namna Wanazi walitesa Mashahidi wa Yehova. Wakati video ilionyesha namna Wanazi walikamata watoto Mashahidi 800 na kuwapeleka mbali na wazazi wao, Maud alisimamisha video. Na alianza kusoma mambo yenye watoto tatu kati ya wale watoto walisema. Kisha kuonyesha ile video, Maud alimalizia kwa kusoma barua ya kuaga ya mwaka 1940 yenye Shahidi moya wa miaka 19 wa Austria, Gerhad Steinacher, aliandikia wazazi wake saa kidogo tu mbele auawe na Wanazi. *

 Maud alizungumuzia ileile habari na wanafunzi wa somo ya pili. Juu ya uhodari wa Maud, wale walimu wote wawili hawasahau kuzungumuzia Mashahidi wa Yehova wakati wanafundisha kuhusu wale wenye waliteswa mu kambi za mateso za Wanazi.

^ Wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu, Mashahidi wa Yehova wa Alemanye, wenye walijulikana pia kuwa Bibelforscher (Wanafunzi wa Biblia), walifungwa juu walikatala kuunga mukono Wanazi.

^ Gerhard Steinacher alihukumiwa kifo juu alikatala kujiunga na jeshi ya Alemanye. Mu barua yake ya kuaga, aliandika hivi: “Ningali mutoto. Naweza kuvumilia kama tu Bwana ananipatia nguvu, na njo yenye ninamuomba.” Asubui yenye ilifuata, Gerhard aliuawa. Maneno yenye iliandikwa ku kaburi yake ilisema hivi: “Alikufa juu ya kumuletea Mungu sifa.”