Ona video zinazopatikana

Mashahidi wa Yehova Wanatumia Namna Gani Michango?

Mashahidi wa Yehova Wanatumia Namna Gani Michango?

 Tunatumia michango juu ya kutegemeza kazi za kidini na kazi za kutoa misaada za tengenezo yetu. Tunaona ile kuwa sehemu kubwa ya kazi yetu ya kusaidia watu wafikie kuwa wanafunzi wa Kristo Yesu.​—Matayo 28:19, 20.

 Hatutumiake michango juu ya kufanya mutu akuwe tajiri. Hatulipe wazee ao mutumishi wowote wa Yehova, na Mashahidi wa Yehova hawalipiwake juu ya kuenda kuhubiri nyumba kwa nyumba. Wale wenye kutumika ku biro za tawi na ku makao yetu makubwa, kutia ndani wale wenye wanafanyiza Baraza Yenye Kuongoza, wako mu shirika ya kidini na hawapatake mushahara wowote.

Mifano Fulani ya Kazi Yetu

  •   Kuchapisha: Tunatafsiri, tunachapisha, tunasafirisha, tunagawanya mamilioni ya Biblia na vichapo vingine vya Kikristo kila mwaka, ile yote bila kulipisha makuta yoyote. Vilevile, site yetu ya jw.org na application yetu ya JW Library inafanya vichapo vyetu vipatikane bila kulipa na bila kufanya matangazo ya biashara juu ya kupata makuta.

  •   Kujenga na Kutunza Majengo: Tunajenga na kutunza nafasi za ibada mu dunia yote juu makutaniko iweze kukutana pamoya fasi ya muzuri ili kumuabudu Mungu. Tunajenga na kutunza pia biro za tawi na biro za kutafsiri. Kazi mingi inafanywa na wajitoleaji na ile inasaidia kupunguza garama.

  •   Usimamizi: Kazi yetu yenye inafanywa ku makao yetu makubwa, biro za tawi, na ku biro za kutafsiri, na hata kazi yenye inafanywa na watumishi wa Yehova wenye kusafiri, inategemezwa na michango ya kujipendea ya mu dunia yote.

  •   Kuhubiri: Mashahidi wa Yehova hawalipiwake juu ya kuhubiri habari njema ao juu ya kufundisha wengine “neno la Mungu.” (2 Wakorinto 2:17) Lakini, sawa vile ilikuwa kwa Wakristo wa karne ya kwanza, watumishi wenye kuchaguliwa na kuzoezwa wenye wanatumia wakati yao mingi mu kazi ya kuhubiri wanapewa fasi ya kuishi na mambo ya musingi yenye wako nayo lazima ili kuishi.​—Wafilipi 4:16, 17; 1 Timoteo 5:17, 18.

  •   Kufundisha: Mikusanyiko yetu inategemezwa na michango ya kujipendea. Tena, tunafanya programu za audio na za video zenye zinategemea Biblia. Tuko pia na masomo ya kuzoeza wazee na watumishi wa wakati yote juu wakuwe na matokeo ya muzuri mu kazi yao.

  •   Kutoa Misaada Wakati ya Misiba: Tunatolea chakula, maji, na nyumba wale wenye walipatwa na misiba yenye kujitokeza na yenye kutokezwa na wanadamu. Hii kazi ya kutoa misaada hailetee faida tu wale wenye kuwa “Mashahidi” lakini pia wale wenye hawako Mashahidi.​—Wagalatia 6:10.