Ona video zinazopatikana

Mashahidi wa Yehova Wanafanyaka Kazi ya Umisionere?

Mashahidi wa Yehova Wanafanyaka Kazi ya Umisionere?

 Ndiyo. Fasi yote kwenye tunaishi, siye Mashahidi wa Yehova wote tunapendaka kufanya kazi ya umisionere; tunafanyaka vile kwa kuambia watu wenye tunakutana nao juu ya imani yetu.​—Matayo 28:19, 20.

 Zaidi ya ile, Mashahidi fulani wanatembelea ao kuhamia fasi ingine mu inchi yao kwenye watu wako na lazima ya kusikia habari njema yenye kuwa Biblia. Mashahidi wengine wanahamia mu inchi ingine juu wahubri sana. Wako na furaha ya kutimiza unabii wenye Yesu alitoa: “Mutakuwa mashahidi wangu . . . mupaka kwenye sehemu ya mbali zaidi ya dunia.”​—Matendo 1:8.

 Mu mwaka wa 1943, tulianzisha masomo fulani juu ya kuzoeza wamisionere wetu. Tangu ile wakati, Mashahidi wa Yehova zaidi ya 8 000 walishasoma ku ile masomo, yenye inaitwa Masomo ya Biblia ya Gileadi.