Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

CreativeDesignArt/DigitalVision Vectors via Getty Images

MUENDELEE KUKESHA!

Inawezekana Watu wa Rangi Zote za Ngozi Watendewe Sawasawa?​—Biblia Inasema Nini?

Inawezekana Watu wa Rangi Zote za Ngozi Watendewe Sawasawa?​—Biblia Inasema Nini?

 Leo, watu wengi wanaona kama haiwezekane watu wa rangi zote za ngozi watendewe sawasawa.

  •   “Mu dunia yote, ubaguzi wa rangi uko sawa vile sumu yenye inaharibisha matengenezo, vikundi vya watu, na maisha ya kila siku ya watu. Unafanya watu waendelee kutendeana bila haki.”​—António Guterres, katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa (secrétaire général des Nations unies).

 Kuko siku yenye watu wa rangi zote watatendewa sawasawa? Biblia inasema nini?

Mawazo ya Mungu juu ya kutendewa sawasawa kwa watu wa rangi zote

 Biblia inafundisha namna Mungu anaona watu wa rangi zote.

  •   “[Mungu] alifanya kila taifa la watu ili wakae juu ya uso wa dunia yote.”​—Matendo 17:26.

  •   “Mungu hana ubaguzi, lakini katika kila taifa mutu mwenye anamuogopa na kufanya mambo yenye kuwa sawa anakubaliwa naye.”​—Matendo 10:34, 35.

 Biblia inaonyesha kama watu wote ni familia moya na kama Mungu anakubali watu wa kila rangi.

Itawezekana kweli watu wa rangi zote watendewe sawasawa?

 Wakati Ufalme wa Mungu, ni kusema, serikali ya mbinguni, utaanza kutawala dunia, watu wa rangi zote watatendewa sawasawa. Ile serikali itafundisha watu namna ya kutendea wengine kwa haki. Watu wataachana kabisa na ubaguzi wa rangi wenye pengine wako nao leo.

  •   “Wakaaji wa inchi [watajifunza] kuhusu haki.”​—Isaya 26:9.

  •   “Matokeo ya haki ya kweli yatakuwa amani, na matunda ya haki ya kweli yatakuwa utulivu wa kudumu na usalama wa kudumu.”​—Isaya 32:17.

 Leo, Biblia iko nafundisha mamilioni ya watu namna ya kutendea wengine muzuri na kwa heshima.