Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Ikiwa Kingsley Anaweza, Mimi pia Ninaweza!”

“Ikiwa Kingsley Anaweza, Mimi pia Ninaweza!”

KINGSLEY iko na chombo kwenye mabega cha kumusaidia kusikia, na anasoma Biblia ili kutoa kipindi chake cha kwanza kwenye Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi katika kutaniko. Anatamuka kila neno vizuri, bila hata kuruka herufi moja. Lakini, sababu gani anasoma bila kuangalia katika Biblia yake?

Kingsley ni kipofu katika inchi ya Sri Lanka. Iko pia na matatizo ya kusikia na ana lazima ya kinga ya vilema ili aweze kutembea. Namna gani mwanaume huyo alijifunza juu ya Yehova na kufikia kustahili kuandikwa kwenye Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi? Acha niwaelezee.

Wakati nilikutana na Kingsley kwa mara ya kwanza, nilishangaa kuona namna alikuwa anapenda kweli ya Biblia. Alikuwa amejifunza Biblia na Mashahidi wengi, na kitabu chake Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele katika maandishi ya Braille, kilikuwa chenye kuzeeka sana. * Wakati nilimuambia tuanze tena kujifunza Biblia pamoja naye, alikubali; lakini tulipambana na matatizo mawili.

Kwanza, Kingsley aliishi pamoja na watu wengine wengi katika nyumba ya kuwatunzia wazee na walemavu. Kwa sababu kulikuwa fujo nyingi katika nyumba hiyo, na Kingsley alikuwa na magumu ya kusikia, nilipaswa kupandisha sauti sana. Kwa hiyo, kila mutu katika nyumba hiyo angeweza kusikia mambo yenye tulikuwa tunajifunza kila juma!

Pili, wakati wa kila funzo, Kingsley hakuwa na uwezo wa kusoma na kujifunza mambo mengi mapya. Ili afaidike kabisa na funzo, alikuwa anajitayarisha muzuri. Mbele siku ya kujifunza ifike, alisoma tena na tena habari ya kujifunza, alisoma maandiko katika Biblia yake ya Braille, na aliweka katika akili majibu ya maulizo. Kufanya hivyo kulileta matokeo mazuri. Wakati wa funzo, Kingsley alikaa kwenye mukeka (kilako); na kwa sababu alifurahia mambo yenye alijifunza, aliyasema kwa sauti kubwa sana. Mwanzoni, tulikuwa tunajifunza mara mbili kwa juma, na kila funzo lilifanya saa mbili!

KUHUZURIA MIKUTANO NA KUTOA MAELEZO

Kingsley na Paul

Kingsley alitamani sana kuhuzuria mikutano kwenye Jumba la Ufalme, lakini haikuwa mwepesi. Alikuwa na lazima ya mutu wa kumutia na kumutosha katika kinga yake, katika motokari, na katika Jumba la Ufalme. Hata hivyo, wengi katika kutaniko walibadilishana ili kumusaidia, na waliona kwamba ni pendeleo kufanya hivyo. Wakati wa mikutano, Kingsley alikaa karibu na kikuza-sauti, na kusikiliza kwa uangalifu, na kutoa hata maelezo!

Kisha kujifunza kwa muda fulani, Kingsley aliamua kujiandikisha kwenye Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi. Juma mbili mbele ya kutoa kipindi chake cha kwanza, nilimuuliza ikiwa alikuwa anafanya mazoezi. Alisema kwa uhakika hivi: “Ndiyo, Ndugu, nimefanya mazoezi mara 30 hivi.” Nilimushukuru kwa sababu ya bidii yake na nilimuomba anisomee. Alifungua Biblia yake na kutia vidole vyake kwenye maandishi ya Braille, kisha akaanza kusoma. Lakini, nilitambua kwamba vidole vyake havikutembea pamoja na maandishi ya Braille. Alikuwa ameweka katika akili yake sehemu ya Biblia yenye aliombwa kusoma!

Machozi ilinitoka na sikuamini mambo yenye niliona. Nilimuuliza Kingsley namna gani aliweza kukumbuka mambo yenye alisoma kisha kufanya mazoezi mara 30 tu. Aliniambia hivi: “Hapana, nilifanya mazoezi mara 30 hivi kila siku.” Kwa zaidi ya mwezi moja, Kingsley alikaa kwenye mukeka na kusoma tena na tena mupaka akaweka katika akili sehemu yenye aliombwa kusoma.

Kisha, siku ilifika ili atoe mugawo wake kwenye Jumba la Ufalme. Wakati alimaliza kusoma, kutaniko lote lilipiga mikono kwa furaha, na wengi walilia kwa kuona bidii ya mwanafunzi huyo mupya. Muhubiri mumoja mwanamuke, mwenye kwa sababu ya wasiwasi, alikuwa ameacha kutoa migawo kwenye masomo, aliomba aandikishwe tena. Sababu gani? Muhubiri huyo alisema hivi: “Ikiwa Kingsley anaweza, mimi pia ninaweza!”

Kisha kujifunza Biblia kwa muda wa miaka tatu, Kingsley alijitoa kwa Yehova na kubatizwa katika maji tarehe 6 Mwezi 9, 2008. Kingsley alibakia mwaminifu mupaka kifo chake tarehe 13 Mwezi wa 5, 2014. Shahidi huyo wa Yehova, alikuwa hakika kwamba katika Paradiso duniani, ataendelea kumutumikia Mungu na nguvu zote na afya kamilifu. (Isa. 35:5, 6)—Habari hii ilielezwa na ndugu Paul McManus.

^ fu. 4 Kilichapishwa katika mwaka wa 1995; leo hakichapishwe tena.