Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kusoma mingi na kuwa na makuta kutafanya ukuwe na maisha ya muzuri wakati wenye kuja?

Kusoma mingi na kuwa na makuta kutafanya ukuwe na maisha ya muzuri wakati wenye kuja?

Watu wengi wanawaza kama wale wenye wanasoma mingi na kuwa matajiri watakuwa na maisha ya muzuri wakati wenye kuja. Wanaamini kama ikiwa mutu anaenda ku université atakuwa mufanyakazi muzuri, atakuwa mutu muzuri mu familia yake na atakuwa mutu wa maana kwa wengine. Pengine wanawaza pia kama kusoma mingi kutawasaidia kuwa na kazi ya muzuri na yenye kulipa muzuri na kama wale wenye kutafuta makuta mingi watakuwa na furaha.

UAMUZI WENYE WENGI WANAKAMATA

Fikiria maelezo ya Zhang Chen, mwenye kuishi Chine. Anasema hivi: “Niliamini kama nilikuwa na lazima ya kusoma université juu nitoke mu umaskini na kama kuwa na kazi yenye kulipa makuta mingi ingenisaidia nikuwe na furaha na maisha ya muzuri.”

Juu wakuwe na maisha ya muzuri watu wengi wanapenda kusoma ku universités zenye kujulikana sana. Wengine wanaenda hata kusomea mu inchi zingine. Watu wengi walizoea kufanya vile mupaka wakati coronavirus ilifanya ikuwe nguvu sana kwa watu kusafiri. Tangu miaka kumi hivi, tengenezo fulani ilifanya uchunguzi na ilitoa ripoti yenye kuonyesha kama “zaidi ya nusu (ao 52 %) ya wanafunzi wenye walikuwa nasoma mu inchi zingine, walikuwa watu wa Asia.”

Mara mingi wazazi wanatumika sana juu watoto wao wasome ku université mu inchi ingine. Qixiang wa Taiwan, anasema hivi: “Wazazi wangu hawakukuwa matajiri. Lakini walitutuma siye watoto ine tuende kusomea mu Amerika.” Juu ya kulipa ili kusoma masomo ya vile, familia yao, sawa vile familia mingi zingine, walipaswa kuwa na madeni mingi.

MATOKEO NI NINI?

Wengi wenye wanajikaza kusoma mingi na kuwa na utajiri wanafikiaka kuvunjika moyo

Mu njia fulani masomo inaweza kutusaidia mu maisha, lakini kila mara hailetake matokeo yenye wanafunzi wanatazamiaka. Kwa mufano, kisha kutumika sana kwa miaka mingi na kukamata madeni mingi juu ya kulipa masomo, wengi hawakuweza kupata kazi yenye walikuwa wanapenda. Ripoti moja ya Rachel Mui mwenye kutumika ku Business Times mu Singapore anasema hivi: “Inaendelea kuwa nguvu sana kwa wale wenye walipata diplome ku université kupata kazi.” Jianjie, mwanaume moja mwenye alisoma masomo mingi, mwenye kuishi Taiwan anasema hivi: “Watu wengi hawapatake kazi yenye inapatana na mambo yenye walisomea.”

Wale wenye wanaweza kupata kazi yenye inapatana na mambo yenye walisomea, pengine wanaweza kuona kama hawapate maisha yenye walitazamia. Kisha kusoma masomo yake ya université Ulaya, Niran, mwenye anaishi Tailandi, alipata kazi ya mambo yenye alisomeaka. Anasema hivi: “Kama vile nilikuwa natazamia, diplome yangu ilinisaidia kupata kazi yenye kulipa makuta mingi sana. Lakini, juu nipate ile makuta mingi iliniomba nitumike sana na kutumia wakati mingi. Ku mwisho kompanyi iliachisha watu wengi kazi na hata miye. Nilitambua kama hakuna kazi yenye inaweza kufanya maisha yetu ya wakati wenye kuja ikuwe muzuri.”

Hata watu wenye kuwa na makuta mingi sana na wenye wanaonekana kama wako na maisha ya muzuri wanaendelea kuwa na magumu mu familia, magumu ya afya na mahangaiko juu ya makuta. Katsutoshi, wa Japani anasema hivi: “Nilikuwa na makuta mingi sana, lakini sikukuwa na furaha juu wengine walikuwa wananisikilia wivu na walikuwa nanitendea mubaya.” Lam, mwanamuke moja mwenye kuishi mu Vietnam, anasema hivi: “Watu wengi wanajikaza sana kutafuta makuta juu wanawaza kama itawafanya wakuwe na maisha ya muzuri, lakini mara mingi wanahangaika sana na hata wanafikia kugonjwa na kushuka moyo.”

Sawa vile Franklin, wengi walifikia kusema kama kuko jambo ya maana zaidi mu maisha kuliko tu kusoma mingi na kuwa na utajiri. Kuliko kukaza akili juu ya kupata vitu vya kimwili watu fulani wanatafuta kuwa na maisha ya muzuri wakati wenye kuja kwa kujikaza kuwa mutu muzuri na kufanyia wengine mambo ya muzuri. Je, kufanya vile kunaweza kuwasaidia wakuwe na maisha ya muzuri wakati wenye kuja? Habari yenye kufuata inatoa jibu.