Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MUNARA WA MULINZI Na. 1 2023 | Afya ya Akili​—⁠Biblia Inaweza Kukusaidia

Magonjwa ya akili ni tatizo yenye kuenea mu dunia yote na iko natesa mamilioni ya watu. Inaweza kupata watu wa miaka, desturi, rangi, kabila, ao dini yoyote. Inaweza kupata wenye walisoma ao wenye hawakusoma, na pia maskini ao matajiri. Afya ya akili ni nini, na inahangaisha watu namna gani? Hii gazeti itazungumuzia faida ya kupata matunzo yenye kufaa na namna Biblia inaweza kusaidia mu njia mbalimbali wale wenye wako na ile matatizo.

 

Magonjwa ya Akili Ni Tatizo Yenye Kuenea mu Dunia Yote

Magonjwa ya akili inaweza kupata watu wa miaka yote na wenye kuwa mu hali yoyote. Ona namna mashauri ya Biblia inaweza kukusaidia ukuwe na afya ya muzuri ya akili.

Mungu Anakuhangaikiaka

Juu ya nini ukuwe hakika kama Yehova Mungu anaelewaka muzuri zaidi mawazo yako na namna uko najisikia kuliko mutu mwingine yeyote?

1 | Sala—“Mumutupie Mahangaiko Yenu Yote”

Kweli tu unaweza kumuambia Mungu mambo yote yenye kukuhangaisha ao kukuogopesha? Namna gani sala inaweza kusaidia wale wenye kuwa na mahangaiko?

2 | “Faraja Kutoka Katika Maandiko”

Biblia inatupatia tumaini ya kweli. Inaonyesha kama hivi karibuni mawazo yenye kuumiza haitakuwa tena.

3 | Mifano ya Biblia Inaweza Kukusaidia

Habari za wanaume na wanamuke wenye kuwa mu Biblia wenye walikuwa na hisia kama zetu zinaweza kutusaidia tusijisikie kuwa pekee yetu wakati tuko na mahangaiko ya mingi.

4 | Biblia Iko na Mashauri Yenye Kusaidia

Ona namna kufikiri juu ya maandiko ya Biblia na kujiwekea miradi yenye unaweza kufikia kunaweza kukusaidia upiganishe matatizo ya akili.

Namna ya Kusaidia Wale Wenye Wako na Matatizo ya Akili

Kama unasaidia rafiki mwenye kuwa na matatizo ya akili, ile inaweza kumufariji na kumutia moyo.