Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Chombo cha udongo cha umbo ya muviringo chenye kuwa na jina Belshaza

Ulijua?

Ulijua?

Namna gani vitu vyenye vilivumbuliwa vinahakikisha kama Belshaza alikuwa mufalme wa Babiloni?

KWA miaka mingi, watu wenye kuchambua Biblia walisema kama Mufalme Belshaza, mwenye kutajwa mu kitabu cha Danieli, hakuishi hata kidogo. (Da. 5:1) Waliamini vile kwa sababu watu wenye kuchimbua vitu vya zamani hawakupata ushuhuda wenye kuonyesha kama aliishi kabisa. Lakini, mawazo yao ilibadilika mu mwaka wa 1854. Juu ya nini?

Katika mwaka huo, balozi mumoja wa Uingereza mwenye kuitwa John Geoge Taylor alichunguza mabomoko fulani mu muji wa zamani wa Uru, wenye kuwa sasa kusini mwa Iraki. Kule, katika munara mukubwa, alipata vyombo fulani vya udongo vya umbo ya muviringo. Kila chombo kati ya vyombo hivyo ine kilikuwa na santimetre 10, na vyombo hivyo vilikuwa na maandishi ya umbo ya pembe (ya Waashuru, Wamedi na Waajemi). Maandishi yenye ilikuwa ku chombo kimoja cha udongo cha umbo ya muviringo kati ya vyombo hivyo ilikuwa sala ya kumuombea Mufalme Nabonido maisha murefu yeye na Belshaza, mwana wake mukubwa. Hata wachambuzi walipaswa kukubali kama vyombo hivyo vya udongo vya umbo ya muviringo vyenye vilivumbuliwa vinahakikisha kama Belshaza aliishi kabisa.

Lakini, Biblia haiseme tu kama Belshaza aliishi lakini inasema pia kama alikuwa mufalme. Juu ya jambo hilo pia, wachambuzi wa Biblia walikuwa na mashaka. Kwa mufano, karibu na mwaka wa 1875, William Talbot, mwanasayansi Muingereza, aliandika kama watu fulani wanasema kama “Bel-sar-ussur [Belshaza] alitawala wakati mumoja na Nabonido baba yake. Lakini, juu ya jambo hilo, hakuna ushuhuda hata kidogo.”

Lakini, ile mabishano ilimalizwa wakati maandishi juu ya vyombo vingine vya udongo vya umbo ya muviringo ilionyesha kama wakati fulani Mufalme Nabonido, Baba ya Belshaza, hakukuwa katika muji mukubwa wa Babiloni. Ni nini ilitokea wakati hakukuwa anaishi mu muji mukubwa? Kitabu kimoja (Encyclopaedia Britannica) kinasema hivi: “Wakati Nabonido alikuwa katika inchi ingine, alimuachia Belshaza kiti cha ufalme na sehemu kubwa ya jeshi lake.” Kwa hiyo, Belshaza alikuwa pia kama vile mufalme wakati huo. Njo maana watu wenye kuvumbua vitu vya zamani na Alan Millard, mutu mwenye elimu ya luga, walisema kama, hakuna kosa ikiwa “kitabu cha Danieli kinamuita Belshaza kuwa ‘mufalme.’”

Kwa kweli, kwa watu wa Mungu, ushuhuda mukubwa wenye kuonyesha kama kitabu cha Danieli ni chenye kutumainika na kiliongozwa na roho ya Mungu unapatikana mu Biblia yenyewe.​—2 Ti. 3:16.