Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ugonjwa wa Nyama Inayoshika Meno—Unaweza Kuupata?

Ugonjwa wa Nyama Inayoshika Meno—Unaweza Kuupata?

UGONJWA huo ni moja kati ya magonjwa ya kinywa ambayo watu wengi wanapata katika ulimwengu. Lakini, katika hatua zake za kwanza kwanza ugonjwa huo hauonyeshe alama mara moja. Hali hiyo hatari ya kutokuonyesha alama ni kati ya mambo yanayojulikana kuhusu ugonjwa huo. Gazeti moja linataja ugonjwa huo kati ya magonjwa ya kinywa ambayo ni “hatari kubwa kwa afya ya watu wote.’’ Gazeti hilo linaongeza kwamba ugonjwa huo unaweza kuwaletea “watu maumivu na mateso na kuwafanya wasifurahie chakula na maisha.” Kuzungumuzia ugonjwa huo wenye kuenea kunaweza kukusaidia ujilinde na ugonjwa huo wa nyama inayoshika meno. (International Dental Journal)

Kweli Kuhusu Ugonjwa wa Nyama Inayoshika Meno

Kuna hatua mbalimbali za ugonjwa wa nyama inayoshika meno. Hatua ya kwanza ni kuvimba kwa nyama hiyo. Wakati nyama inayoshika meno inatosha damu, hilo linaonyesha kwamba hatua hiyo imeanza. Damu inaweza kutoka wakati mutu anasukua meno kwa kutumia muswaki ao kamba ao inaweza kujitokea yenyewe. Tena, ikiwa damu inatoka wakati nyama inayoshika meno inachunguzwa na muganga, hilo linaweza kuonyesha kwamba nyama inayoshika meno imevimba.

Hatua ya kufuata ya ugonjwa huo inaitwa periodontite. Wakati ugonjwa unafikia hatua hiyo, viungo vya kinywa vinavyotegemeza meno, kama vile mifupa na nyama inayoshika meno inaanza kuharibika. Wakati fulani hatua hii haionyeshe alama yoyote mupaka wakati itafikia hatua mbaya zaidi. Alama fulani za periodontite zinaweza kuwa mianya katika meno; meno yenye kuregea; mashimo katikati ya meno; harufu mbaya ya kinywa; nyama za meno zenye kuachana na meno, na kufanya meno ionekane kuwa murefu; na kutoka kwa damu.

Mambo Yanayoleta Ugonjwa Huo na Matatizo Yake

Kuna mambo mengi yanayoweza kufanya mutu apate ugonjwa wa nyama inayoshika meno. Jambo kubwa zaidi ambalo linafanya watu wapate ugonjwa huo ni utando wa meno ambao ni kitu chembamba chenye kujaa mikrobe ambacho kinakuwa kwenye meno kila siku. Ikiwa utando huo hauondolewe, mikrobe iliyo kwenye utando wa meno inaweza kufanya nyama inayoshika meno ivimbe. Hatua hiyo inapoendelea, nyama inayoshika meno inaweza kuanza kuachana na meno, na hilo linafanya utando wa meno wenye kujaa mikrobe uingie chini ya nyama inayoshika meno. Kisha mikrobe kuingia ndani ya nyama inayoshika meno, ugonjwa huo unaendelea na kuharibu mufupa na nyama inayoshika meno. Iwe utando wa meno uko juu ao chini ya nyama inayoshika meno, unaweza kugeuka na kuwa majiwe madogo-madogo magumu yanayoitwa kalkulasi. Sehemu hizo ngumu zinafunikwa pia na mikrobe, na kwa sababu ziko ngumu na zinashika sana meno, haziondolewe kwa vyepesi. Kwa hiyo, mikrobe inaweza kuendelea kuharibu sana nyama inayoshika meno.

Kuna mambo mengine yanayoweza kufanya upate ugonjwa wa nyama inayoshika meno. Mambo hayo yanatia ndani kukosa kusafisha vizuri kinywa, kutumia dawa zinazozuia mufumo wa kulinda mwili na magonjwa usitumike vizuri, kuambukizwa na virusi, kuhangaika kwa akili, ugonjwa wa sukari, kunywa pombe kupita kiasi, kuvuta tumbako, na mabadiliko ya homoni yanayotokana na mimba.

Ugonjwa wa nyama inayoshika meno unaweza kukuletea matatizo mengine. Kinywa chenye kuuma ao kupoteza meno kwa sababu ya ugonjwa wa nyama inayoshika meno unaweza kufanya iwe vigumu kutafuna na kufurahia chakula. Unaweza kuwa na matatizo ya kuongea na sura yako haitapendeza. Tena, uchunguzi umeonyesha kama kusafisha vizuri kinywa kuna matokeo mazuri juu ya afya ya mwili wote.

Kutambua na Kutunza Ugonjwa wa Nyama Inayoshika Meno

Namna gani unaweza kujua kama umepata ugonjwa huo? Unaweza kutambua alama fulani ambazo tayari tumezungumuzia katika habari hii. Ikiwa unatambua hilo, ni jambo la hekima uonane na muganga mwenye ufundi wa kutunza meno ambaye anaweza kuchunguza hali za nyama inayoshika meno yako.

Inawezekana kutunza ugonjwa huo? Ugonjwa huo unaweza kupona ikiwa unatunzwa wakati uko katika hatua zake za mwanzo-mwanzo. Ikiwa ugonjwa wa nyama inayoshika meno unaendelea mupaka kuanza kutoa usaha, basi inaomba kuzuia ugonjwa huo mbele uharibu mufupa na nyama ambazo zinazunguka meno. Waganga wa meno wanatumia vifaa vya hali ya juu ambavyo vinaweza kuondoa utando wa meno na sehemu ngumu zinazofunika meno, juu ao chini ya nyama inayoshika meno.

Hata ikiwa unaweza kupata matunzo fulani ao hauwezi kupata matunzo ya kutosha ya magonjwa ya meno, jambo la maana ambalo litakusaidia uepuke ugonjwa huo unaoshambulia mutu kwa siri ni kuchukua mipango ya kujilinda. Kutunza kinywa chako vizuri na kwa ukawaida ndio njia nzuri sana ya kupunguza uwezekano wa kupata ugonjwa wa nyama inayoshika meno.