Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Umeambukizwa na Tabia ya Ubaguzi?

Umeambukizwa na Tabia ya Ubaguzi?

Ubaguzi uko kama ugonjwa wenye kuambukiza. Unaumiza wale wenye wameambukizwa nao, na watu wanaweza kuambukizwa nao bila hata kujua.

Watu hawabaguwake wengine juu tu ya inchi yao, rangi yao ya ngozi, kabila yao, ao luga yao. Lakini pia wanabaguwaka wengine juu ya dini yao, hali yao ya maisha, ao juu ni mwanaume ao mwanamuke. Watu fulani wanabagua wengine juu ya miaka yao, elimu yao, ulemavu wao, ao juu ya namna wanaonekana kwa inje. Hata kama wanafanya ile mambo yote, wanajisikia kama hawana ubaguzi.

Ulishaambukizwa na ubaguzi? Wengi kati yetu wanaweza kuona kama wengine njo wako na ubaguzi. Lakini, inaweza kuwa nguvu kujua kama tuko na ubaguzi. Ukweli ni kuwa, sisi wote tunakuwaka na ubaguzi kwa kiasi fulani. Profesa wa sosholojia, David Williams, anasema kama “wakati watu wako na mawazo ya mubaya juu ya kikundi fulani na wakati wanakutana na mutu fulani wa kile kikundi wanamutendeaka kwa ubaguzi na wanafanya vile bila hata wao kujua.”

Kwa mufano, katika inchi ya Balkani kwenye Jovica anaishi, kuko kikundi cha watu kidogo. Anasema hivi: “Niliwaza kama watu wote wenye kuwa mu kile kikundi hawako watu wazuri. Lakini, sikuona kama ile ni ubaguzi. Nilijiambia hivi: ‘Njo vile tu wanakuwaka.’”

Serikali mingi zinaweka sheria juu ya kupiganisha ubaguzi wa rangi ya ngozi na aina zingine za ubaguzi. Hata kama wanafanya vile, ubaguzi unaendelea. Juu ya nini? Ni juu zile sheria zinahukumu tu matendo ya ubaguzi. Hazina mamlaka juu ya mawazo ya mutu na juu ya namna mutu anajisikia. Na ni mu moyo na mu akili ya mutu njo mwenye ubaguzi unaanziaka. Tunaweza kupiganisha ubaguzi na kupata ushindi? Je, kuko dawa ya ubaguzi?

Habari zenye kufuata zitazungumuzia kanuni tano zenye zinaweza kusaidia watu wengi wapiganishe mawazo ya ubaguzi yenye wako nayo.