Ona video zinazopatikana

Biblia Inasema Nini Kuhusu Ndoa Kati ya Watu wa Rangi Mbalimbali?

Biblia Inasema Nini Kuhusu Ndoa Kati ya Watu wa Rangi Mbalimbali?

Jibu la Biblia

 Mungu anakubali ndoa kati ya mwanaume na mwanamuke wa rangi tofauti kwa sababu rangi zote ziko sawa machoni pake. Biblia inasema hivi: “Mungu hana ubaguzi.”—Matendo 10:34, 35, Habari Njema kwa Watu Wote.

 Ona kanuni fulani za Biblia zinazohusu ndoa na usawa ulio kati ya watu wa rangi mbalimbali.

Rangi zote zilitokana na mutu mumoja

 Wanadamu wote ni wazao wa mwanaume wa kwanza, Adamu, na bibi yake, Eva, ambaye Biblia inaita ‘mama ya kila mutu anayeishi.’ (Mwanzo 3:20) Ni kwa sababu hiyo, Biblia inasema hivi: ‘Kutokana na mutu mumoja, aliumba mataifa yote.’ (Matendo 17:26, Habari Njema kwa Watu Wote) Hata wawe wa rangi gani, wanadamu wanafanyiza familia moja tu. Lakini, unaweza kufanya nini ikiwa kuna ubaguzi mwingi mahali unapoishi?

Watu wenye hekima ‘wanashauriana pamoja’

 Mungu anakubali ndoa kati ya watu wa rangi tofauti. Lakini, watu wote hawana maoni kama yake. (Isaya 55:8, 9) Ikiwa unafikiria kufunga ndoa na mutu wa rangi nyingine, wewe na yule unayetaka kufunga naye ndoa munapaswa kufikiria pamoja maulizo haya:

  •   Mutapambana namna gani na mikazo inayoweza kutoka kwa watu wa eneo lenu ao familia yenu?

  •   Namna gani mutawasaidia watoto wenu wapambane na ubaguzi?

 ‘Kushauriana pamoja’ kunaweza kuwasaidia muwe na ndoa nzuri.—Methali 13:10; 21:5.