Ona video zinazopatikana

MUSAADA KWA FAMILIA

Wakati Mawazo Inapingana

Wakati Mawazo Inapingana

Kupendezwa na mambo tofauti, kuwa na tabia na utu wenye kuwa tofauti kunaweza kuleta matatizo ya nguvu kati ya bibi na bwana wenye kuoana. Lakini mambo ingine inaweza kuleta matatizo ya nguvu zaidi. Kwa mufano:

  • Mutapitisha muda gani pamoja na watu wa jamaa

  • Namna ya kutumia feza

  • Mutazaa watoto ao hapana

Unaweza kufanya nini ikiwa wewe na bibi ao bwana yako muko na mawazo yenye kupingana?

 Mambo unapaswa kujua

Kupatana hakumaanishe kufanana. Hata bibi na bwana wenye kupatana sana hawatakuwa na mawazo ileile kila wakati, hata juu ya mambo ya maana sana.

“Nilikomalia mu familia yenye umoja sana. Kila mwisho wa juma, tulikuwa tunapitisha wakati pamoja na wazazi wa mama na baba, ndugu za baba yangu, wajomba, shangazi, na binamu. Lakini, katika familia ya bwana yangu hawakuzoea kufanya mambo mingi pamoja. Kwa hiyo, tuko na mawazo yenye kupingana juu ya muda wenye tunapaswa kupitisha pamoja na watu jamaa ao juu ya wakati wa kuongea na watu wa jamaa wenye kuishi mbali sana.”​—Tamara.

“Kwa sababu ya namna tulikomaa, mimi na bibi yangu tulikuwa na mawazo yenye kupingana juu ya namna ya kutumia feza. Katika miezi ya kwanza-kwanza ya ndoa yetu, tulikuwa na mabishano kidogo juu ya jambo hilo. Iliomba tuzungumuze mara mingi ili tufikie kuelewana.”​—Tyler.

Watu wawili wanaweza kuangalia tukio moja lakini kila mutu anaweza kuelewa tukio hilo kwa namna yake. Ni vile pia juu ya jambo lenye bibi na bwana hawakubaliane juu yake

Matatizo fulani haiwezi kumalizwa kwa kukubaliana kuiacha tu. Tuseme nini kama mutu fulani wa familia ya bibi ao ya bwana yako anagonjwa na iko na lazima ya matunzo? Ao tuseme nini kama bibi ao bwana anapenda kuzaa watoto lakini mwingine hapendi? a

“Mimi na bibi yangu hatukuzungumuzia sana juu ya kuzaa watoto. Anaendelea kuwaza sana juu ya jambo hilo, na mawazo yetu inaendelea kuwa tofauti. Sione namna tunaweza kuelewana.”​—Alex.

Kuwa tu na mawazo yenye kuwa tofauti hakumaanishe kama ndoa yenu itavunjika. Watu fulani wenye elimu wanasema kama ikiwa wewe na bibi ao bwana yako hamuwezi kupatana juu ya tatizo fulani la nguvu sana, unapaswa kufanya nguvu yako yote ili upate kile chenye unataka, hata kama inaomba kuvunja ndoa yenu. Lakini, kumaliza magumu kwa njia hiyo, kunaonyesha kama unaona mawazo yako kuwa ya maana sana na unazarau naziri yenye ulifanya mbele ya Mungu kama utashikamana na bibi ao bwana yako hata kutokee nini.

 Mambo unaweza kufanya

Uazimie kuheshimia naziri yako ya ndoa. Kama munaazimia kuheshimia naziri yenu ya ndoa, hilo litawasaidia mutumike pamoja ili kumaliza magumu yenu.

Kanuni ya Biblia: “Kile chenye Mungu ameunganisha, mutu yeyote asikitenganishe.”​—Matayo 19:6.

Uhesabie garama. Kwa mufano, wazia kuwa bibi ao bwana anapenda kuzaa watoto lakini mwingine hapendi. Kuko mambo mingi ya kufikiria, kwa mufano:

  • Ndoa yenu iko na nguvu kwa kadiri gani.

    Mutaweza kupambana na mahangaiko ingine yenye kuletwa na kukomalisha watoto?

  • Madaraka ya kuwa muzazi.

    Daraka la wazazi haiko tu kutolea watoto chakula, nguo, na nafasi ya kuishi.

  • Feza zenye muko nazo.

    Utaweza kuwa na usawaziko kati ya kazi, familia, na madaraka ingine?

Kanuni ya Biblia: “Ni nani kati yenu mwenye akitaka kujenga munara hakae kwanza na kuhesabia garama?”​—Luka 14:28.

Fikiria mambo yote juu ya tatizo fulani. Munaweza kufikia kuelewana juu ya mambo fulani. Kwa mufano, ikiwa tatizo ni kuzaa watoto ao hapana, bibi ao bwana mwenye hapendi anaweza kujiuliza hivi:

  • ‘Wakati ninasema kama sipendi kuzaa watoto, maana yake sipendi kuzaa hata siku moja ao sipendi kuzaa kwa sasa?’

  • ‘Sipendi kuzaa kwa sababu sijue kama ninaweza kuwa muzazi muzuri?’

  • ‘Ninaogopa kama bibi ao bwana yangu ataacha kunihangaikia?’

Kwa upande mwingine, bibi ao bwana mwenye anapenda kuzaa anapaswa kufikiria maulizo kama hii:

  • ‘Tuko tayari kutimiza madaraka ya muzazi?’

  • ‘Tuko na feza za kukomalisha mutoto?’

Kanuni ya Biblia: “Hekima yenye inatoka juu . . . ni . . . yenye usawaziko.”​—Yakobo 3:17.

Tambua kama mawazo ya bibi ao bwana yako inaweza kuwa na faida. Watu wawili wanaweza kuangalia tukio moja lakini kila mutu anaweza kuelewa tukio hilo kwa namna yake. Vilevile, mu ndoa, bibi na bwana wanaweza kuwa na mawazo yenye kuwa tofauti juu ya namna ya kushugulikia jambo fulani kwa mufano, juu ya namna ya kutumia feza. Wakati munazungumuzia jambo lenye kila mumoja wenu iko na mawazo tofauti juu yake, muanze na mawazo yenye munakubaliana.

  • Muko na miradi gani yenye kupatana?

  • Wazo la kila mumoja liko na faida gani?

  • Ili kuokoa ndoa yenu, mumoja wenu ao ninyi wawili munaweza kubadilisha mawazo yenu ili muelewane?

Kanuni ya Biblia: “Kila mumoja aendelee kutafuta, hapana faida yake mwenyewe, lakini faida ya ule mutu mwingine.”​—1 Wakorinto 10:24.

a Mambo mazito inapaswa kuzungumuziwa mbele ya kufunga ndoa. Lakini hali zenye hazitazamiwe zinaweza kutokea, ao mawazo ya bibi ao bwana inaweza kubadilika kadiri wakati unapita.​—Muhubiri 9:11.