Hamia kwenye habari

Video za Biblia​—Mafundisho Muhimu

Masomo haya mafupi ya video yanajibu maswali muhimu ya Biblia. Baadhi ya video hizi zinahusiana na masomo yaliyo katika broshua Habari Njema Kutoka kwa Mungu!

Je, Ulimwengu Uliumbwa?

Mara nyingi simulizi la Biblia la uumbaji hueleweka vibaya au wengine huliona kuwa hekaya. Je, kile ambacho Biblia inasema kinapatana na akili?

Je, Mungu Ni Halisi?

Chunguza uthibitisho unaoonyesha kwamba ni jambo linalopatana na akili kuamini Mungu yupo.

Je, Mungu Ana Jina?

Mungu ana majina mengi ya cheo, kama vile, Mweza-Yote, Muumba, na Bwana. Lakini jina la kibinafsi la Mungu limetumiwa mara 7,000 hivi katika Biblia.

Je, Inawezekana Kuwa Rafiki ya Mungu?

Kwa karne nyingi, watu wametambua kwamba wanahitaji kumjua Muumba wao. Biblia inaweza kutusaidia kuwa rafiki ya Mungu. Urafiki huo unaanza kwa kujifunza jina la Mungu.

Ni Nani Aliyeitunga Biblia?

Ikiwa Biblia iliandikwa na wanadamu, je ni sahihi kuiita Neno la Mungu? Biblia ina mawazo ya nani?

Tunawezaje Kuwa na Hakika Kwamba Yale Yaliyoandikwa Katika Biblia Ni ya Kweli?

Ikiwa Biblia ilitungwa na Mungu, haipaswi kuwa kama kitabu kingine kilichowahi kuandikwa.

Kwa Nini Mungu Aliiumba Dunia?

Dunia imejaa vitu maridadi. Iko umbali unaofaa kabisa kutoka kwenye jua, imeinama kwa pembe inayofaa kabisa, na inazunguka kwa mwendo unaofaa kabisa. Kwa nini Mungu alifanya jitihada kubwa sana hivyo kuiumba dunia?

Maisha Yana Kusudi Gani?

Tafuta siri ya kupata furaha ya kweli na kusudi maishani.

Wafu Wako Katika Hali Gani?

Biblia inaahidi kwamba kuna wakati ambapo watu wengi watafufuliwa, kama tu Lazaro alivyofufuliwa.

Je, Watu Watateswa Katika Moto wa Mateso?

Biblia inatuambia kwamba kwa sababu “Mungu ni upendo,” hawezi kamwe kuwatesa watu kwa sababu ya makosa yao ya zamani.

Je, Yesu Kristo Ni Mungu?

Je, Yesu Kristo ndiye Mungu Mweza-Yote? Au ni watu wawili tofauti?

Kwa Nini Yesu Alikufa?

Huenda unajua kwamba alikufa kwa sababu ya dhambi zetu? Lakini dhabihu ya mtu mmoja inawezaje kuwanufaisha mamilioni ya watu?

Ufalme wa Mungu Ni Nini?

Wakati wa huduma yake duniani, Yesu alifundisha kuhusu Ufalme wa Mungu kuliko habari nyingine yoyote. Kwa karne nyingi, wafuasi wake wamesali kwamba Ufalme huo uje.

Ufalme wa Mungu Ulianza Kutawala 1914

Zaidi ya miaka 2,500 iliyopita, kupitia roho ya Mungu mfalme mwenye nguvu alipata ndoto ya kinabii inayotimia sasa.

Ulimwengu Umebadilika Tangu 1914

Hali na mitazamo ya ulimwengu tangu 1914 inaonyesha wazi kwamba unabii wa Biblia kuhusu “siku za mwisho” unatimizwa.

Je, Misiba ya Asili Ni Matendo ya Mungu?

Watu wawili walioathiriwa na misiba ya asili wanaeleza mambo waliyojifunza kutoka katika Biblia.

Kwa Nini Mungu Anaruhusu Kuteseka?

Biblia inajibu kwa njia yenye kuridhisha na yenye kufariji.

Je, Mungu Anakubali Aina Zote za Ibada?

Watu wengi wanaamini kwamba dini unayochagua si jambo la maana.

Je, Mungu Anakubali Sanamu Zitumiwe Katika Ibada?

Je, zinaweza kutusaidia kujihisi karibu na Mungu asiyeweza kuonekana?

Je, Mungu Husikiliza Sala Zote?

Vipi ikiwa mtu anatoa sala yenye ubinafsi? Namna gani ikiwa mume anamtendea mke wake vibaya halafu anamwomba Mungu ambariki?

Mungu Ana Maoni Gani Kuhusu Ndoa?

Mungu anataka ndoa yako iwe na furaha. Ushauri mzuri unaopatikana katika Biblia umewasaidia wenzi wengi wa ndoa.

Je, Ponografia Ni Dhambi Machoni Pa Mungu?

Je, neno “ponografia” linapatikana katika Biblia? Tunawezaje kujua maoni ya Mungu kuhusu ponografia?